Sunday, December 6

KIDUME NDANI.... Kim Kardashian na Kanye West waongeza furaha ndani ya familia yao…

Ni habari njema kwa familia ya Rapper wa Marekani Kanye West na mke wake Kim Kardashian!!.
Baada ya safari ndefu ya ujauzito wa staa huyo wa kipindi cha televisheni cha ‘Keeping Up with the Kardashians’ ambayo ilichukua headlines katika vyombo mbalimbali vya habari duniani hatimaye familia ya mastaa hao imejaliwa mtoto wa pili wa kiume jana Desemba 5.
Mtoto huyo ambaye mpaka sasa hajapewa jina anakuwa ni mdogo wa mtoto wao wa kwanza aitwaye North West.

No comments: