Saturday, October 8

Body Parts You Didn’t Know Had Names! 0

Glabella. The glabella is the space between the eyebrows. A glabellar reflex is a primitive reflex found in patients with Parkinson’s disease. When repeatedly tapped on the forehead, they blink continuously. Normal people do not.

HIZI HAPA KURASA ZA MBELE NA NYUMA ZA MAGAZETI YA LEO OKT 8/2016

ZSSF TENDER : PROVISION OF CLEANING SERVICES AT ZSSF PREMISES, ZANZIBAR

ZANZIBAR SOCIAL SECURITY FUND
                                                                P.OBOX 2716,
                                                KILIMANI MNARA WA MBAO,
                                                                  ZANZIBAR

Tender No. ZSSF/2016/2017/NC/01
For
Provision of Cleaning Services at ZSSF Premises, Zanzibar

 

Friday, October 7

KUHUSU HALI YA HEWA KWA LEO NA KESHO TANZANIA

MINISTRY OF WORKS, TRANSPORT AND COMMUNICATION

TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY-TMA

P.O.BOX 3056, DAR ES SALAAM
Tel / fax. 2460772.
LAKE VICTORIA ZONE.
WEATHER FORECAST FOR THE NEXT 24 HOURS STARTING AT 9.00PM, 07/10/2016
This forecast is for Mwanza, Kagera, Mara and Shinyanga regions.

DR.MAGUFULI ATISHIA KUMFUTA KAZI MTOTO WA DADA YAKE KWA KISA HIKI.................


Rais Dkt John Pombe Magufuli ametishia kufukuza kazi mtoto wa dada yake kutokana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutopeleka umeme katika kiwanda kipya cha kusindika matunda cha Bakhresa.

CHAMA CHA WANANCHI {CUF} HATARINI KUFUTWA


Mgogoro unaoiandama CUF huenda ukailetea balaa zaidi, baada ya kuwapo kwa taarifa kuwa huenda ikafutwa kama itazidi kukomalia msimamo ilionao wa kutotaka ushauri.

RUSSIA YAIONYA VIKALI MAREKANI, YASEMA HAIWEZI KUKABILIANA NA S300, S400

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Russia, Igor Konashenkov amesema kuwa, shambulio lolote la kombora au la anga litakalolenga maeneo ya jeshi la serikali ya Syria, litakuwa linahatarisha majeshi ya Russia na Syria kwa pamoja.
Konashenkov ameitaka Marekani kuzingatia kwa umakini matokeo mabaya yatakayotokana na hatua yake ya kushambulia maeneo ya jeshi la Syria.
Msemaji wa Wizara ya Ulinzi nchini Russia, Igor Konashenkov.
Ameingeza kuwa, baada ya hujuma ya anga iliyofanywa na ndege za kivita za Marekani tarehe 17 Septemba dhidi ya jeshi la  Syria, Moscow ilichukua hatua za lazima za kuzuia kujikariri tukio kama hilo dhidi ya jeshi lake nchini Syria.

WAFANYABIASHARA WA DRC WAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA.

k1
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Congo (DRC) nchini Tanzania Bw. Sumail Edward (kulia) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari kuhusu uamuzi wa wafanyabiashara wa Congo kutumia Bandari ya Dar es Salaam baada ya Serikali kuondoa vikwazo, kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari  Bw. Tiganya Vincent.
k2
Baadhi ya waandishi wa habari wakimfuatilia kwa makini Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Congo (DRC) nchini Tanzania Bw. Sumail Edward (mwenye suti) wakati alipokuwa akielezea kuridhika na uamuzi wa Serikali ya Tanzania kuondoa vikwazo katika Bandari ya Dar es Salaam na kupelekea wafanyabiashara wa Congo (DRC) kuendelea kuitumia bandari hiyo.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MADUDU MAMLAKA YA USTAWISHAJI MAKAO MAKUU DODOMA (CDA)


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Bunge), Bw. Uledi Mussa afuatilie malipo ya kiwanja kilichouzwa na CDA kwa sh. milioni 240 lakini fedha iliyoingia ofisini ni sh. milioni 6 tu.

LIGI YA WANAWAKE KUANZA KUTIMUA VUMBI NOVEMBA MOSI, TIMU 12 KUSHIRIKI


Timu 12 zinatarajiwa kushiriki Ligi ya Taifa ya Wanawake inayotarajiwa kuanza Novemba mosi, mwaka huu kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Maendeleo ya Soka la Wanawake na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), zilizoridhia tarehe hiyo.

COLOMBIAN PRESIDENT JUAN MANUEL SANTOS WINS NOBEL PEACE PRIZE


Colombian President Juan Manuel Santos was awarded the Nobel Peace Prize for his efforts to bring the country’s 52-year old conflict with the FARC rebels to an end. 
Santos had managed to secure a peace deal with the FARC rebels, although it was voted down in a referendum less than a week ago.

Thursday, October 6

RIDHIWANI ASAIDIA MAGODORO 50 MORETO BAADA YA BWENI KUUNGUA

more
BWENI la wanafunzi wasichana katika shule ya sekondari ya Moreto iliyopo tarafa ya Msoga wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, baada ya kuungua kwa moto na kusababisha mali zote za wanafunzi hao kuteketea kwa moto. (Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
MBUNGE wa jimbo la Chalinze, mkoani Pwani, Ridhiwani Kikwete, ametoa magodoro 50, yenye thamani ya sh.mil 2.225 kwa wanafunzi wa kike wa shule ya sekondari Moreto, waliounguliwa na bweni lao na kusababisha mali zote kuteketea kwa moto.
Wanafunzi hao wapatao196, katika shule hiyo iliyopo kata ya Lugoba tarafa ya Msoga, wilaya ya Bagamoyo, wamenusurika kifo baada ya bweni hilo kuteketea kwa moto siku ya october 5.
Moto huo umeteketeza mali zote zilizokuwemo ambazo hadi sasa hazijajulikana thamani yake.
Kufuatia kutokea kwa tukio hilo, Ridhiwani alifika shuleni hapo kutembelea na kutoa pole kwa kutokea janga hilo.
Alisema wakumshukuru ni mungu kwani pamoja na kutokea kwa hasara ya kuteketea kwa mali lakini hakuna madhara kwa wanafunzi yaliyotokea.
Ridhiwani aliwapa pole walimu na wanafunzi kijumla na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kwenda kusaidia pale watakapojaaliwa.
Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Moreto, Justine Lyamuya alielezea kuwa, tukio hilo limetokea October 5,majira ya asubuhi ambapo walianza kuona moshi mzito katika bweni mojawapo wanaloishi wasichana wa shule hiyo.
Alisema wakati moto huo unazuka wanafunzi hao walikuwa kwenye masomo yao darasani.
“Tulifuatilia na kukuta moto umeshashika kwenye bweni hilo na jitihada za kuuzima zilishindikana”alisema mwalimu Lyamuya.
Lyamuya alisema mali zote za wanafunzi wanaolala kwenye bweni hilo zimeteketea kwa moto hivyo kwa sasa wanafanya tathmini kujua gharama zilizopotea.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, alielezea kuwa mazingira ya jengo hilo ni yenye kutumia nishati ya solar power hivyo ni lazima kufanya uchunguzi wa kina kujua kiini cha kuzuka kwa moto huo.
Alisema bweni hilo linakadiriwa kuwa na wanafunzi 196.
Kamanda Mushongi alisema thamani za mali za wanafunzi katika moto huo bado hazijafahamika.