Thursday, December 17

Hawa Ndo Top 5........Wajue wasanii watano wenye ushawishi mkubwa Africa kwa mwaka 2015… Mtanzania yupo mmoja tu!...


Nimekutana na jarida la New African Magazine toleo ya December 2015 na ndani ya jarida hilo nikakutana na list ya watu waliotajwa kama watu wenye ushawishi mkubwa zaidi Africa kwa mwaka huu wa 2015… kwa upande wa burudani nimekutana na mastaa watano huku Mtanzania akiwemo mmoja tu!
AAAAA
Hawa ndio Africa Most Influencial Africans in Media, Arts & Culture waliotajwa na jarida la New African Magazine:
Lupita Nyong’o – Kenya.
Baada ya kushinda tuzo yake ya kwanza ya Oscars ya Best Supporting Role kwenye filamu yake ya kwanza kubwa, Two Years A Slave, staa wa movie Lupita Nyong’o kutoka Kenya amezidi kuonyesha uwezo wake kwenye industry ya filamu Marekani kwa kuzidi kupokea nafasi nyingi kubwa za kuigiza pamoja na kushinda tuzo kadhaa kwenye majukwa mbalimbali Marekani. Licha ya hayo Lupita pia ni Balozi wa Wild Elephants na Mwanaharakati wa haki za Wanyama.
African1
Lupita Nyong’o.
Trevor Noah – South Africa.
Mchekeshaji kutoka South Africa, Trevor Noah aliiteka  dunia baada ya Marekani kumtangaza kuwa mtangazaji mpya atakayerithi kiti cha show ya comedy, The Daily Show nchini Marekani. Toka ujio wa Trevor Noah kwenye kipindi hicho watazamaji wa show hiyo kutoka Marekani wametokea kuvutiwa na mchekeshaji huyo ambaye material yake kubwa ya comedy inaongelea sehemu kubwa ya maisha ya Kiafrika. Kwa mujibu wa ripoti kadhaa zilizotolewa na mitandao tofauti Marekani, ujio wa Trevor Noah kwenye kipindi hicho kumeongeza watazamaji milion 1.5 kwenye show hiyo.
African2
Trevor Noah.
Diamond Platnumz – Tanzania.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva na mshindi wa tuzo ya MTV Africa Music Awards 2015: Best Live Act pamoja na MTV EMA 2015: Best African Act, Diamond Platnumz kwa mwaka huu ametajwa kama mmoja wa wasanii wa kubwa wa Africa kwa mwaka 2015 akiwa na ushawishi mkubwa ndani na nje ya Africa, akiwa pia na mashabiki wakubwa na wanaomuongelea zaidi kwenye mitandao ya kijamii kitendo kinachomfanya Diamond kuwa msanii kijana mwenye ushawishi mkubwa kwa mwaka huu wa 2015.
african3
Diamond Platnumz.
Yemi Alade – Nigeria
Baada ya hit song yake ya ‘Johnny’ kuweka headlines sehemu mbalimbali Africa staa wa muziki kutoka Nigeria, Yemi Alade alijipatia umaarufu mkubwa sana kupitia video hiyo ambayo ushawishi wake umegusa watazamaji zaidi ya milion 30 kweye mtandao wa YouTUBE. Ukiachia hayo style yake ya muziki pamoja na mavazi yake imetokea kuvutia wasichana wengi wanaofuatilia muziki wake.
African4
Yemi Alade.
Koffi Olomide – DRC Congo.
Mkongwe wa muziki kutoka Congo, Koffi Olomide amekuwa akijulikana kwenye industry ya muziki kuanzia miaka ya 1970 na bado umaarufu wake unagusa watu wengi wa rika zote duniani. Mwezi October mwaka huu 2015, Koffi aliachia album yake ya 13 na ya mwisho ikiwa na nyimbo 39. Licha ya kuachia Album yake ya mwisho Koffi anahesabika kama miongoni ya watu waliobadilisha sura ya muziki nchini Congo.
Africa5
Koffi Olomide.

Dhamana Yatolewa Kwa Vigogo TRA.....

Hatimaye vigogo watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) akiwemo kamishna wa forodha na ushuru wa mamlaka hiyo, Tiagi Masamaki wameachiwa dhamana na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa mahakama kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam.

YAMEMKUTA..haya Baada ya Vichapo Vingi......Jose Mourinho afutwa kazi Chelsea....

Meneja wa klabu ya Chelsea ya Uingereza amefutwa kazi baada ya klabu hiyo kuandikisha msururu wa matokeo mabaya.

The Blues walishinda Ligi ya Premia msimu uliopita lakini msimu huu mambo yamekuwa kinyume, na wamo alama moja tu juu ya eneo la kushushwa daraja ligini.
Bodi ya klabu hiyo ilikutana jana kujadili hatima ya Mourinho chini ya mmiliki wa klabu hiyo, Mrusi Roman Abramovich.
Klabu hiyo kupitia taarifa imesema mkataba kati ya klabu na meneja hiyo umekatishwa kwa maelewano kati ya pande zote mbili na ikamtakia kila la kheri Mourinho.
“Sifa zake Stamfrod Bridge na Uingereza zinajieleza na daima anakaribishwa kurejea Stamford Bridge,” klabu hiyo imesema kupitia taarifa.
“Sasa tutaangazia kuhakikisha kikosi chetu kilichojaa wachezaji wenye vipaji kinafikia uwezo wake. Hakutakuwa na taarifa zozote zaidi kutoka kwa klabu hadi kocha mpya ateuliwe.”
Mreno huyo mwenye umri wa miaka 52 amekuwa Chelsea kwa kipindi cha pili, kilichoanza Juni 2013.
Chelsea walimaliza alama nane mbele kileleni msimu uliopita na kutwaa taji pamoja na Kombe la Ligi lakini mwaka huu wameanza vibaya, wakishindwa mechi tisa kati ya 16 ligini kufikia sasa.
Mechi ya mwisho kwa Mourinho kwenye usukani ilikuwa Jumatatu walipochapwa na viongozi wa ligi Leicester City 2-1.
Mourinho alitia saini mkataba mpya wa miaka minne tarehe 7 Agosti mwaka huu na ndiye meneja aliyefanikiwa zaidi akiwa na Chelsea.
Alishinda mataji matatu ya Ligi ya Premia kipindi chake cha kwanza katika klabu hiyo kati ya 2004 na 2007.
Pep Guardiola, Guus Hiddink, Brendan Rodgers na Juande Ramos na miongoni mwa wanaopigiwa upatu kumrithi.

ETI NAYEE NI MUUZA UNGA....Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya ya Nelly yafutwa...


nelly
Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya iliyomkabili rapa Nelly imefutwa. Nelly ametoa tamko juu ya swala hili na kusema
“Namshukuru wakili wangu Scott Rosenblum na watu wa mji wa Tennessee kwa kuwa na haki juu yangu”
Nelly alikamatwa Tennessee mwezi wa nne na polisi wa usalama barabarani na kukutwa na aina ya paraphernalia,marijuana na mfuko mwingine wenye methamphetamine ambao baada ya vipimo iligundulika kuwa haikuwa dawa ya methamphetamine.
Nelly alifikishwa mahakamani na kukubali kosa la kukutwa na dawa hizo na alipewa adhabu ya kifungo cha nje cha mwaka mzima.

KASI YA HAPA KAZI TU.....DC MAKONDA kawageukia wakandarasi wa barabara..Kuna ufisadi?...


Ile kauli ya Rais kuhakikisha anapunguza matumizi yasiyo yalazima kwa Serikali imeendelea kuchukua headlines, pia tumeshuhudia baadhi ya viongozi wakisimamishwa kazi kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma
Leo Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda amewageukia wakandarasi wa barabara za Manispaa yake ambao imeonekana wametumia kiasi cha fedha za umma kinyume na makubaliano.
Barabara nyingi zimejengwa chini ya kiwango...”Vita kubwa tuliyonayo ni ya matumizi mabaya ya pesa za umma, mwaka huu niliunda kamati ya kuchunguza barabara, matokeo yake wakatupa picha kuwa barabara zetu zimejengwa chini ya kiwango, nimekuja kwenu leo nikiwa na mambo makubwa matatu, ujenzi wa miradi ya barabara kuna pesa mbayo huongezeka kutokana na sababu kadhaa ambayo inatakiwa isizidi 15 ya pesa iliyopitishwa katika mkataba wa awali”..Paul Makonda.
Makandarasi kutolipwa kuanzia sasa“Nimezuia kuanzia sasa hakuna wakandarasi watakaolipwa katika hizi barabara sita, na nimeagiza siku tano nipate taarifa na nimeelekeza kuandika barua kwa Mkurugenzi, na mafaili yalete ofisini kwake, wale watakaobanika watachukulia hatua kali za kisheria”….
Fedha zimetolewa kinyume na utaratibu..“Fedha zilizotengwa kwa ajili ya kujenga barabara sita za Manispaa ya Kinondoni ni bilioni 4.9 ndio pesa iliyopitishwa, lakini fedha iliyoongozeka ni bilioni 5.7 ambayo haipo kwenye mkataba, zaidi ya bilioni 10 zinahitajika kwa mradi uliopaswa kujengwa kwa bilioni 4..Bodi ya wazabuni walitembelea miradi baada ya kuona wanaomba pesa, walikuta  miradi haipaswi kuongezewa pesa, walioomba pesa hawajapewa kibali lakini tayari wamelipwa pesa, naitaka hiyo pesa irudishwe haraka iwezekanavyo” Paul Makonda.
“Ziko taratibu za malipo, zinazotolewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara zetu kwa utaratibu unaotakiwa, kwa hali hii nitaendelea kupigana vita daima na sitakatishwa tamaa na kila anayejiunga na mafisadi, kwa mamlaka niliyonayo ninasitisha ulipwaji wa wakandarasi katika barabara za Mkwajuni, Lion, Biafra, Mabatini, Feza road, Mandaz Road, nataka hatua zichukuliwe, wachunguzi wa mahesabu watoe ufafanuzi kwa hizi fedha zilizozidi”Paul Makonda.
“Barabara ya kujengwa kwa milioni 500 inajengwa kwa bilioni1.3 hii sio sawa,tunahitaji fedha katika mambo mbalimbali si kuwatajirisha watu wachache ambao wanaihujumu nchi yetu”. Paul Makonda

Monday, December 14

Zuma amteua waziri mwingine wa fedha...


Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amemteua waziri mwingine wa fedha katika kipindi cha siku nne, baada ya uteuzi wa awali kupingwa vikali.
Bw Zuma alikuwa amemfuta kazi Nhlanhla Nene wiki iliyopita na kumteua Desmond Van Rooyen kuwa waziri mpya.
Hatua hiyo ilipingwa vikali na watu huku masoko yakidorora na thamani ya sarafu ya Rand ikishuka pakubwa.
Uteuzi huo pia ulishutumiwa kupitia mitandao ya kijamii, kitambulisha mada #Zumamustfall kikivuma sana Afrika Kusini.
Kutokana na hayo, Rais Zuma ameamua kubadilisha uamuzi wake na kumteua Pravin Gordon ambaye amewahi kuwa waziri wa fedha.
Bw Gordon ndiye aliyemtangulia Bw Nene katika Hazina Kuu na alisaidia kuongoza taifa hilo kupitia msukosuko wa kudorora kwa uchumi 2009.
Mwandishi wa BBC aliyeko Johannesburg Matthew Davies anasema sarafu ya Rand ilianza kuimarika Jumapili na bei ya hisa katika Soko la Hisa la Johannesburg inatarajiwa kuanza kupanda tena wiki hii.
Hata hivyo, hali ya Bw Zuma kuonekana kutokuwa na msimamo itaathiri sana chama tawala cha ANC huku taifa hilo likijiandaa kwa uchaguz wa serikali za mitaa mwaka ujao.

Zuma amteua waziri mwingine wa fedha...


Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amemteua waziri mwingine wa fedha katika kipindi cha siku nne, baada ya uteuzi wa awali kupingwa vikali.
Bw Zuma alikuwa amemfuta kazi Nhlanhla Nene wiki iliyopita na kumteua Desmond Van Rooyen kuwa waziri mpya.
Hatua hiyo ilipingwa vikali na watu huku masoko yakidorora na thamani ya sarafu ya Rand ikishuka pakubwa.
Uteuzi huo pia ulishutumiwa kupitia mitandao ya kijamii, kitambulisha mada #Zumamustfall kikivuma sana Afrika Kusini.
Kutokana na hayo, Rais Zuma ameamua kubadilisha uamuzi wake na kumteua Pravin Gordon ambaye amewahi kuwa waziri wa fedha.
Bw Gordon ndiye aliyemtangulia Bw Nene katika Hazina Kuu na alisaidia kuongoza taifa hilo kupitia msukosuko wa kudorora kwa uchumi 2009.
Mwandishi wa BBC aliyeko Johannesburg Matthew Davies anasema sarafu ya Rand ilianza kuimarika Jumapili na bei ya hisa katika Soko la Hisa la Johannesburg inatarajiwa kuanza kupanda tena wiki hii.
Hata hivyo, hali ya Bw Zuma kuonekana kutokuwa na msimamo itaathiri sana chama tawala cha ANC huku taifa hilo likijiandaa kwa uchaguz wa serikali za mitaa mwaka ujao.

ICTR kutoa hukumu ya mwisho leo...


Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) iliyokuwa ikishughulikia kesi za mauaji yaliyotokea miaka 20 iliyopita leo itatoa hukumu yake ya mwisho kabla ya kufungwa kabisa.
Hukumu hiyo itakuwa dhidi ya watuhumiwa Pauline Nyiramasu ambaye ni waziri wa zamani wa Maendeleo ya wanawake nchini Rwanda na mtoto wake ambaye wote wamekana mashtaka yanayowakabili.
Mahakama hiyo ambayo imekuwako Kaskazini mwa Tanzania katika mji wa Arusha ilikuwa ikisikiliza kesi za watuhumiwa wa mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.
Mara kadhaa waendesha mashtaka wa mahakama hiyo walikabiliwa na mashahidi waliokuwa tayari kutoa ushahidi.
Hata hivyo mafanikio yake yamepongezwa na watu wengi ambao wamesema si rahisi kuwatafuta na kushtaki watuhumiwa wote.

Raia wa Marekani kuondoka Burundi...



Serikali ya Marekani imeshauri Raia wake walio nchini Burundi kuondoka nchini humo haraka iwezekanavyo baada ya watu 87 kuuawa kwenye ghasia zilizotokea siku ya Ijumaa.
Ghasia zilizojitokeza kwenye mitaa ya mji mkuu wa nchi hiyo, Bujumbura ni mbaya zaidi tangu kuanza kwa vurugu mwezi Aprili baada ya Rais Pierre Nkurunziza kuamua kuwania tena urais kwa muhula wa tatu.
Shirika la kutetea haki za kibinadamu la Human Rights Watch (HRW) limeitisha uchunguzi kuhusu mauaji hayo ya Ijumaa.
Mwezi uliopita, Ubelgiji pia iliwashauri raia wake kuondoka Burundi, huku Muungano wa Ulaya (EU) nao ukipunguza wahudumu wake, kwa kuondoa wafanyakazi ambao ni wa muda, "familia na wafanyakazi ambao si muhimu sana."
"Kufuatia machafuko ambayo yanaendelea kuongezeka, Wizara ya Kigeni meagiza kuondoka kwa jamaa za maafisa wa Marekani na maafisa ambao si wa kushughulikia dharura nchini Burundi," taarifa ya Marekani ilisema.
"Ubalozi wa Marekani unaweza kutoa huduma za dharura kwa kiwango cha chini tu kwa raia wake nchini Burundi."
Jijini Nairobi, wanaharakati Jumapili jioni waliwakusanya vijana kutoka Burundi, Kenya na nchi nyingine za Afrika Mashariki jijini Nairobi kwa ajili ya mkesha na kuwasha mishumaa kuwakumbuka Raia wa Burundi walioathirika kutokana na mzozo wa kisiasa nchini mwao.
Aidha, walitoa wito kwa jamii ya kimataifa kuingilia kati.

TP Mazembe yachapwa 3 - 0 Klabu Bingwa Duniani....


Wawakilishi wa Afrika katika michuano ya kombe la dunia la vilabu timu ya Tp Mazembe imechapwa na wenyeji wa michuano hiyo timu ya Sanfrecce Hiroshima 3-0.
Wenyeji Hiroshima walipata mabao yao kupitia Tsukasa Shiotani, Dakika ya 44, Kazuhiko Chiba, 56, na Takuma Asano, akifunga bao la mwisho.
kipigo hicho kinainyima nafasi timu ya Tp Mazembe kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo hivyo watachuana na Klabu America, ya Mexico, ambayo nayo ilichapwa kwa mabao 2-1 Guangzhou Evergrande.
Kwenye nusu fainali Sanfrecce Hiroshima, watawachuana na River Plate, huku Barcelona wakikipiga na Guangzhou Evergrande.

YALIYOJIRI LEO.....Magazeti ya Tanzania December 14 2015 na stori zake kubwa kurasa za mwanzo na mwisho......

Leo December 14 2015 nimekuwekea tena stori zote kubwa za Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye Udaku, michezo na hardnews ili ujue kinachoendelea Mtanzania....
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.