Huenda ukawa umezoea na kuboreka na foleni ya jiji la Dar Es Salaam ambalo wakati mwingine inaweza kukugharimu kwa zaidi ya saa moja kukaa katika foleni kutoka Tegeta hadi Posta, hususani mvua ikiwa inanyesha Dar Es Salaam sehemu huwa zinakuwa na foleni kubwa. Mtu wangu wa nguvu nimekutana na list ya mpya kutoka www.telegraph.co.uk ya miji 10 inayoongoza kwa foleni Duniani, imeandikwa 04/02/2016.
Friday, February 26
SOMA YA LEOOO.....Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo February 26 2016 kwenye udaku, hardnews na michezo....
Thursday, February 25
PATA HII.....TOKA IKULU YA TANZANIA.....
Ikulu imeahidi kufanyia kazi madai ya Chama cha Wasanii Wachoraji
Tanzania (Chawata), ambayo waliyawasilisha jana, kikilalamikia ofisi
hiyo katika awamu ya nne iliyokuwa chini ya Rais Jakaya Kikwete,
kuwachelewa malipo yao ya Sh. milioni 53.6.
SOMA HII......TANZANIA na "Cash Budget"......
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli, imeamua kutumia
mfumo wa ‘Cash Budget (kutumia kilichokusanywa), huku baadhi ya wachumi
wakisema utaleta nidhamu ya matumizi ya serikali na kubana watumishi
ambao walizoea kutumia vibaya fedha za umma kwa kuzipangia matumizi
yasiyo na tija.
Wizara ya Fedha na Mipango imeeleza kuwa, mfumo wa kupanga na kutumia kinachokusanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA), ndiyo ulioamuliwa kutumiwa na serikali ya awamu ya tano.Itakumbukwa kuwa, tangu Novemba mwaka jana, mapato ya TRA yalipanda kutoka wastani wa Sh. bilioni 800 na Sh. bilioni 900 kwa mwezi mpaka Sh. trilioni 1.3, Desemba, mwaka jana Sh. trilioni 1.4, Januari, mwaka huu Sh. trilioni 1.06 na malengo ya Februari ni kukusanya Sh. 1.03.
Jana Ofisa Habari wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ingiaheddi Mduma, alisema utaratibu wa kutumia kilichokusanywa utaendelea kutumika kila mwezi.
Alisema kila makusanyo yatakayopatikana kwa mwezi husika, yatatumika kulingana na mahitaji husika ya mwezi huo.
“ Mahitaji yakiwa mengi katika mwezi husika, basi hata fedha itakayokusanywa kwa mwezi huo itatumika kulingana na mahitaji hayo, tutakuwa tunafanya hivyo kila mwezi,” alisema Mduma.
Wizara ya Fedha na Mipango imeeleza kuwa, mfumo wa kupanga na kutumia kinachokusanywa na Mamlaka ya Mapato (TRA), ndiyo ulioamuliwa kutumiwa na serikali ya awamu ya tano.Itakumbukwa kuwa, tangu Novemba mwaka jana, mapato ya TRA yalipanda kutoka wastani wa Sh. bilioni 800 na Sh. bilioni 900 kwa mwezi mpaka Sh. trilioni 1.3, Desemba, mwaka jana Sh. trilioni 1.4, Januari, mwaka huu Sh. trilioni 1.06 na malengo ya Februari ni kukusanya Sh. 1.03.
Jana Ofisa Habari wa Wizara ya Fedha na Mipango, Ingiaheddi Mduma, alisema utaratibu wa kutumia kilichokusanywa utaendelea kutumika kila mwezi.
Alisema kila makusanyo yatakayopatikana kwa mwezi husika, yatatumika kulingana na mahitaji husika ya mwezi huo.
“ Mahitaji yakiwa mengi katika mwezi husika, basi hata fedha itakayokusanywa kwa mwezi huo itatumika kulingana na mahitaji hayo, tutakuwa tunafanya hivyo kila mwezi,” alisema Mduma.
UTAJIRI WA TANZANIA...
Tanzania imedhihirisha kuwa ni tajiri mkubwa wa rasilimali ya gesi
asilia baada ya kugundulika kwa gesi nyingine katika bonde la mto Ruvu
yenye ukubwa wa ujazo wa futi trilioni 2.17.
Ugunduzi huo wa gesi asilia umefanywa na Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons and Power Tanzania Limited ambayo imekuwa inafanya shughuli za utafutaji wa gesi na mafuta katika Mkoa wa Pwani.Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Pilavullathil Surendran alisema jana katika mkutano wa wawekezaji wa gesi na mafuta ulioandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, thamani ya gesi iliyoko katika eneo hilo inafikia Dola za Marekani bilioni sita sawa na Sh trilioni 12.
Ugunduzi huo mpya unafanya hadi sasa Tanzania kuwa na amana ya gesi yenye ukubwa wa futi za ujazo trilioni 57.27.
Ugunduzi huo wa gesi asilia umefanywa na Kampuni ya Dodsal Hydrocarbons and Power Tanzania Limited ambayo imekuwa inafanya shughuli za utafutaji wa gesi na mafuta katika Mkoa wa Pwani.Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, Pilavullathil Surendran alisema jana katika mkutano wa wawekezaji wa gesi na mafuta ulioandaliwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, thamani ya gesi iliyoko katika eneo hilo inafikia Dola za Marekani bilioni sita sawa na Sh trilioni 12.
Ugunduzi huo mpya unafanya hadi sasa Tanzania kuwa na amana ya gesi yenye ukubwa wa futi za ujazo trilioni 57.27.
PITIA HAPA.....Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo February 25 2016 kwenye udaku, hardnews na michezo.....
Sunday, February 21
SOMA HAPAAAA.....Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo February 21 2016 kwenye, Hardnews na michezo....
February 21 2016 naanza kwa kukusogezea post ya stori zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye , Michezo na haerdnews ili uju kinachoendelea......





Subscribe to:
Posts (Atom)