Thursday, February 25

PATA HII.....TOKA IKULU YA TANZANIA.....

Ikulu imeahidi kufanyia kazi madai ya Chama cha Wasanii Wachoraji Tanzania (Chawata), ambayo waliyawasilisha jana, kikilalamikia ofisi hiyo katika awamu ya nne iliyokuwa chini ya Rais Jakaya Kikwete, kuwachelewa malipo yao ya Sh. milioni 53.6.
 
Kwa mujibu wa taarifa ya Chawata kwa vyombo vya habari jana, fedha hizo zimetokana na kazi za sanaa ambazo zilichukuliwa na serikali ya awamu ya nne kutoka kwa wafanyabiashara wa eneo la Mwenge jijini Dar es Salaam na kupelekwa Ikulu.

Hata hivyo, Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa, alithibitisha kuwapo na madai hayo na kuwa yatafanyiwa kazi ndani ya wiki moja kuanzia jana.

“Ni kweli Ikulu inadaiwa, lakini ni deni la awamu ya nne, kwa hiyo tumewaomba kuwakamilishia madai yao ndani ya wiki moja, baada ya kufanya uhakiki ili kujiridhisha,” alisema Msigwa.

No comments: