Thursday, April 14

POLIS WATATU WATIMULIWA KATI KISHA KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUPOKEA RUSHWA TABORA


Polisi watatu wa wilayani Urambo, Mkoa wa Tabora wamefikishwa mahakamani kwa mashitaka ya kuomba na kupokea rushwa. 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoani Tabora, iliwafikisha askari hao jana katika Mahakama ya Wilaya ya Urambo huku mwingine akidaiwa kukimbia.

Askari hao waliofukuzwa kazi kabla ya kufikishwa mahakamani ni John Okinda, Kabila Pius na Patrick Robart. 

Anayedaiwa kukimbia ni Elisha ambaye polisi inaendelea kumtafuta. 

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Urambo, Hassan Momba, Wakili wa Takukuru, Edsoni Mapalala alidai washitakiwa walitenda makosa hayo Machi 7 mwaka huu.

Mapalala alidai siku hiyo katika kijiji cha Mkirigi, Kata ya Ilege, Wilaya ya Kaliua, washitakiwa hao wakiwa waajiriwa wa jeshi la polisi, waliomba rushwa ya Sh milioni tatu kutoka kwa Dotto Gandulanye ili wasimchukulie hatua za kisheria baada ya kumkuta akiwa na bangi.

BARCELONA NI KAMA SIMBA YA BONGO, YATUPWA NJE UEFA NA MAJIRANI WA MAHASIMU WAO JIJINI MADRID


Hivi majuzi timu y asoka y aSimba SC ya hapa nyumbani iling'olewa katika hatua y arobo fainali katika kombe la FA licha ya mashabiki wengi kuipa nafasi y akushinda kutokana na mwenendo mzuri iliyonayo katika ligi, lakini mbele ya Vijana wa Tanga, {Coastal Union} wakalala mbili moja mwele ya mashaiki wao jijini Dar es salaam.

vivyo hivyo hapo jana usiku Klabu ya soka ya Barcelona Jumatano ilivuliwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Atletico Madrid huku Mabao yote ya Altletico Madrid yakifungwa na Antoine Griez-mann na bao la pili likifungwa kwa mara nyingine na Antoine kwa njia ya penalti .

Kwa matokeo hayo Atletico Madrid wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 3 -2 baada ya awali kufungwa 2-1 na Barcelona katika Uwanja wa Camp Nou.

Katika mchezo mwingine Bayern Munich imefakiwa kutinga nusu fainali baada ya kuitoa Benfica kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya sare ya 2-2 katika mchezo wa jana .

Mabao ya Benfica yamefungwa na Raul Alonso Rodriguez na Anderson Souza Conceicao , na magoli ya Bayern Munich yakifungwa na Arturo Vidal na Thomas Muller .

Hivyo Atletico Madrid na Bayern Munich zinaungana na Real Madrid ya Hispania pamoja na Manchester City katika nusu fainali ambayo droo yake itapangwa siku ya Ijumaa.

Wednesday, April 13

KAMANDA WA POLIS MWANZA AWATAKA POLIS KUWAKABILI MAJAMBAZI KWA NGUVU ZOTE....


Kamanda mpya wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewataka polisi kukabiliana na majambazi kwa nguvu zote na ikibidi kuwaua kabla hawajasababisha madhara makubwa kwa raia.

NEC YAPONGEZWA KWA UCHAGUZI WA 2015 KUMALIZIKA KWA AMANI


Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala imeipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kufanikisha kuendesha Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani wa mwaka 2015 vizuri na kuiacha nchi ikiwa na Amani, utulivu na Usalama.

WANANCHI WATAKIWA KUWAOMBEA VIONGOZI

 

MKE wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa amewaomba wananchi wa wilaya ya Ruangwa kuwaombea dua viongozi wa taifa, Rais Dk. John Magufuli, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ili waweze kufanya kazi zao kikamilifu. 

PICHA !! RAIS MAGUFULI AKIPOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA MABALOZI KUTOKA NCHI MBALIMBALI IKULU

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati ya Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa nchi ya Jamhuri ya Czech hapa nchini Pavel Rezac, tukio hilo lilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.