Friday, October 23

BAADA YA MADAI YA UTOVU WA NIDHAMU HII NDIO KAULI YA DIEGO COSTA

Mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Diego Costa ambaye amekuwa akiingia katika headlines kutokana na baadhi ya matukio yake anayoyafanya uwanjani, October 23 ameingia katika headlines tena baada ya kusema kuwa hawezi kubadilika kutokana na watu wanavyotaka na kufikiria.

Diego Costa amekuwa akiingia katika headlines kutokana na vitendo vyake vya utovu wa nidhamu, Diego Costa tayari alishafungiwa mechi tatu mwaka huu katika vipindi viwili tofauti tofauti. Costa alifungiwa mechi tatu kutokana na kugombana na beki wa Arsenal Laurent Koscielny na kumkanyaga kwa makusudi beki wa Liverpool Emre Can.

“Sitobadilika hivyo kwa sababu ya watu wanavyoweza kufikiria, baadhi ya watu wanaweza kufikiria mchezo wa mpira wa miguu ni kama ukumbi wa michezo kuwa kila mmoja anaweza kufanya vizuri. Lakini nafikiria mtu hubadilika pale unapovuka mstari mweupe wa kuingia uwanjani na unakuwa mtu tofauti na pale unapokuwa nje ya uwanja, ila ninapokuwa uwanjani naenda kupambana kwa ajili ya timu yangu na kuhakisha nafanya vizuri”>>> Diego Costa

No comments: