Monday, October 19

AU YAUNDA JESHI LA PAMOJA AFRIKA



Kikosi kipya cha majeshi ya umoja wa Afrika kinafanya mazoeozi yake ya kwanza hii leo nchini Afrika Kusini.

Mazoezi hayo yanalenga kutathmini utayari wa kikosi hicho kutumika wakati kunapotokea dharura na kunahitajika kikosi cha mbele kitakachodhibiti hali na kuokoa maisha ya watu.

Lakini swali ibuka ni je jeshi hilo litatumwa katika taifa lililochangia wanajeshi wake ?

Mwandishi wa BBC anayeshughulikia maswala ya kiusalama Tomi Oladipo, anasema kuwa madhumuni ya kikosi hicho cha wanajeshi 25,000 kutoka mataifa ya bara Afrika ni kupunguza kutegemea kwa majeshi ya mataifa ya ulaya kuja humu barani kusuluhisha migogoro inayotokea.




Kikosi hicho kinatarajiwa kuanza oparesheni yake ya kwanza mwezi januari mwakani.

Hata hivyo umoja wa Afrika unasema unahitajika takriban dola bilioni moja kufadhili shughuli na oparesheni za kikosi hicho.

Mwandishi wa BBC anayeshughulikia maswala ya kiusalama anasema kuwa kuna changamoto za ukosefu wa ushirikiano mwema baina ya mataifa shirika.




Vilevile anasema kuwa mataifa mengi hayajajitolea kuunga mkono jeshi hilo kisiasa.
Jeshi hilo linatarajiwa kuwa na vikosi vitano.

Kwa sasa Cameroon imejitolea kuwa mwenyeji wa kikosi hicho ikisema watakita kambi yao katika mji wa Douala.

                                             bbcswahili.com 

No comments: