Friday, October 23

MAHAKAMA: MARUFUKU MITA MIAMBILI, PIGA KURA, RUDI NYUMBANI

Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imetoa maamuzi ya kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na kada wa Chadema aliyekuwa akiiomba mahakama hiyo kutoa uamuzi wa kwamba wananchi wanatakiwa kukaa mita ngapi baada ya kupiga kura.


Mahakama hiyo imelitolea suala hilo ufafanuzi na kusema kuwa ni marufuku kwa wananchi kukusanyika katika kituo cha kupigia kura na hata njee ya mita 200 hairuhusiwi kwani ni kinyume cha sheria.


Kesi hiyo namba 37 ya mwaka huu, ilifunguliwa na mgombea ubunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chadema, Amy Kibatala, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) chini ya hati ya kiapo cha dharura.


Oktoba 16, mwaka huu, mlalamikaji alifungua kesi ya kikatiba iliyopewa usajili namba 37, ya mwaka huu akiiomba Mahakama itoe tafsiri ya kifungu cha 104 kidogo cha (1) cha Sheria ya Uchaguzi kama kinazuia ama kuwaruhusu wananchi kukaa kwa utulivu umbali wa mita 200, baada ya kupiga kura katika vituo.

No comments: