Sunday, January 31

BARCA WAINGIA NUSU FAINALI KOMBE LA MFALME



Mabingwa watetezi wa kombe la Mfalme Barcelona wamesonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Barcelona waliwachapa Athletic Bilbao kwa mabao 3-1 kwa mabao ya Luis Suarez, Gerrard Pique na Neymer na hiyo barca kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-2.

Nao Celta de vigo wakawaondoa katika michuano hiyo vijana wa Diego Simione Atletico Madrid kwa kuwachapa kwa mabao 3-2.

Robo fainali ya pili itapigwa leo usiku kwa Las Palmas kushuka dimbani kuwakabili Valencia, huku Mirandés wakiwa na kibarua pevu dhidi ya Sevilla.

No comments: