Sunday, January 31

JAMA ATOA MPYA KWA KUSAFIRI PEKE YAKE KWENYE NDEGE KWA LENGO LA KUTALII


Inaweza kutokea unasafiri kwenye gari hivi labda toka Dar mpaka Morogoro kwenye basi la abiria peke yako, unaweza kujifariji kwa kuchekicheki nje mazingira, ukachezea simu yako au ukaendelea zako na safari kwa kusikiliza muziki au kuangalia TV kwenye basi, lakini vipi kwenye ndege  inakuwaje?

Jamaa mmoja Alex Simon mtalii kutoka Austria, alijikuta kwenye level za kistaa hivi au mtu fulani VIP kwenye ubora wake baada ya kujikuta akiwa ndio abiria pekeake ndani ya ndege ya abiria zaidi ya 100… alitoka zake  Manila kwenda Boracay ndani ya Ufilipino kwa ajili ya kutalii tu !!

Baada ya Simon kuingia kwenye ndege alianza kupiga stori na marubani baadae akaungana na wahudumu wawili wa ndege wakiendelea na stori mpaka alipotua

Cheki Video ya jamaa mwenyewe hii hapa mwanzo mpaka mwisho wa safari.

No comments: