Tuesday, November 24

USINDI SURA MBAYA...SHINDANO LA SURA MBAYA ZIMBABWE LAMALIZIKA KWA GHASIA.....

Ghasia zimeibuka baada ya mwanaume mwenye umri wa miaka 42 kutangazwa kuwa mshindi katika shindano la mtu mwenye sura mbaya Jijini Harare nchini Zimbabwe, huku mashabiki wakiwatuhumu majaji kwa upendeleo.

Majaji hao walimchagua, Mison Sere, kuwa mshindi kutokana na kutokuwa na meno mengi na kuwa na uwezo wa kuibadilisha sura yake kwa kuikunja kunja, na kumshinda bingwa mtetezi William Masvinu, ambaye amekuwa bingwa tangu mwaka 2012.

Mshindi wa shindano la mwanaume mwenye sura mbaya nchini Zimbabwe, huibuka na zawadi ya dola 500, ambayo ni fedha nyingi ukizingatia wengi wa washiriki wa shindano hilo huwa hawana ajira maalum.
                                      Washiriki wa sura mbaya wakiwa katika mapozi tofauti 
                    Mshindi wa shindano la sura mbaya Mison Sere akiwa amebebwa juu

No comments: