Tuesday, February 16

Kutoka kwa...WAZIRI MUHONGO.....

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka wawekezaji katika sekta za nishati na madini kufanya utafiti wa kutosha katika maeneo husika kabla ya kuendelea na miradi yao.Profesa Muhongo aliyasema hayo katika mkutano baina yake na wawakilishi kutoka Kampuni ya Lake Holdings ukiwa ni moja kati ya mikutano kadhaa inayoendelea wiki nzima baina ya Wizara na wawekezaji wa sekta hizo.
Kampuni hiyo iliyosajiliwa mwaka 2012 ina mpango ya kujenga kituo cha kuzalisha umeme chenye uwezo wa megawati 300 hadi megawati 450 wilayani Songea mkoani Ruvuma.
Huo ni mradi mkubwa zaidi ukilinganishwa na mradi wao wa awali katika Kata ya Kiwira wilayani Rungwe, Mbeya uliolenga megawati 200 za umeme.

No comments: