Tuesday, February 16

JIPU LA....MSD..

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amemwagiza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari Kuu ya Dawa (MSD), kuwasimamisha kazi mara moja wakurugenzi wanne wa taasisi hiyo kutokana na tuhuma za kuwepo matumizi mabaya ya Sh bilioni 1.5.
Wakurugenzi hao ni Mkurugenzi wa Kanda wa MSD, Cosmas Mwaifwani, Mkurugenzi wa Fedha, Joseph Tesha, Mkurugenzi wa Ugavi, Misanga Muja na Mkurugenzi wa Manunuzi, Heri Mchunga.“Naomba uwaandikie barua za kuwasimamisha wakurugenzi hawa wanne ili wapishe uchunguzi wa matumizi mabaya ya Sh bilioni 1.5 za MSD,” alisema Ummy alipozungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam.
Ummy alisema taarifa alizonazo ni kwamba kiasi hicho cha fedha, kilitumika kununulia dawa kinyume cha utaratibu na Sheria ya Manunuzi ya Umma, hivyo kuna haja ya kufanyika kwa uchunguzi huo.

No comments: