Monday, February 15

Magazeti ya Tanzania yalichoandika leo February 15 2016 kwenye Hardnews na michezo......


February 15 2016 naanza kwa kukusogezea post ya stori zote kubwa zilizobebwa kwenye Magazeti ya Tanzania kuanzia kwenye Udaku, Michezo na hardnews ili ujue kinachoendelea DSCN0282 DSCN0283 DSCN0284 DSCN0285 DSCN0286 DSCN0287 DSCN0288 DSCN0289 DSCN0290 DSCN0291DSCN0292 DSCN0293 DSCN0294 DSCN0295 DSCN0296 DSCN0297 DSCN0298 DSCN0299 DSCN0300 DSCN0301 DSCN0302 DSCN0303DSCN0304 DSCN0305 DSCN0306 DSCN0307 DSCN0308 DSCN0309 DSCN0310 DSCN0311 DSCN0312 DSCN0313 DSCN0314 DSCN0315DSCN0316 DSCN0317 DSCN0318 DSCN0319 DSCN0320
DSCN0321

Monday, February 1

ALIYESABABISHA GUZMAN KUNASWA AHOJIWA

Mwigizaji filamu wa Mexico Kate del Castillo anahojiwa kuhusiana na sakata inayomhusu mmoja wapo wa walanguzi wakuu wa dawa za kulevya Joaquin "El Chapo" Guzman ambaye sasa anatumikia kifungo gerezani.

Sunday, January 31

Marais wapinga kutuma jeshi la AU Burundi


Image copyright

Muungano wa Afrika AU hautatuma kikosi cha walinda amani hadi pale serikali ya rais Pierre Nkurunziza itakapotoa mwaliko.

Hatariiiii!!!! Mji wafurahia mtoto wa kwanza baada ya miaka 28

Ostina


Image copyright

Mji mmoja kaskazini mwa Italia unasherehekea kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza tangu mapema miaka ya 1980.

Matangazo ya bunduki yapigwa marufuku Facebook

Bunduki


Image copyright

Watu binafsi hawataruhusiwa tena kuweka matangazo ya kuuza bunduki katika Facebook na Instagram, kampuni ya Facebook ambayo pia inamiliki Instagram imetangaza.

Tai wa Israel aliyedhaniwa kuwa jasusi sasa huru

Tai


Image copyright

Tai huyo alitoka Uhispania
Tai mkubwa aliyezuiliwa nchini Lebanon akituhumiwa kuwa jasusi wa Israel ameachiliwa huru baada ya walinda usalama wa Umoja wa Mataifa kuingilia kati, maafisa wa Israel wamesema.

Wawindaji haramu wamuua rubani nchini Tz


Shirika moja la wakfu wa utunzaji wa mazingira, linasema kuwa rubani mmoja raia wa Uingereza, amepigwa risasi na kuuawa nchini Tanzania.
Rubani huyo anasemekana kuwa alikuwa akipepeleza mzoga wa ndovu porini alipodunguliwa na mwindaji haramu aliyekuwa amejificha .
Operesheni hiyo ilikuwa katika mbuga ya wanyama pori ya Maswa Kaskazini mwa Tanzania.

Ugiriki:Wasusia mechi kupinga vifo vya wahamiaji



Image copyright

Wachezaji wa timu mbili hasimu nchini Ugiriki wamesusia mechi wakipinga ongezeko la vifo vya wahamiaji wanaozama wakijaribu kuingia nchioni humo kukwepa vita Syria na Iraq.

BARCA WAINGIA NUSU FAINALI KOMBE LA MFALME



Mabingwa watetezi wa kombe la Mfalme Barcelona wamesonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Barcelona waliwachapa Athletic Bilbao kwa mabao 3-1 kwa mabao ya Luis Suarez, Gerrard Pique na Neymer na hiyo barca kusonga mbele kwa jumla ya mabao 5-2.

Nao Celta de vigo wakawaondoa katika michuano hiyo vijana wa Diego Simione Atletico Madrid kwa kuwachapa kwa mabao 3-2.

Robo fainali ya pili itapigwa leo usiku kwa Las Palmas kushuka dimbani kuwakabili Valencia, huku Mirandés wakiwa na kibarua pevu dhidi ya Sevilla.

JAMA ATOA MPYA KWA KUSAFIRI PEKE YAKE KWENYE NDEGE KWA LENGO LA KUTALII


Inaweza kutokea unasafiri kwenye gari hivi labda toka Dar mpaka Morogoro kwenye basi la abiria peke yako, unaweza kujifariji kwa kuchekicheki nje mazingira, ukachezea simu yako au ukaendelea zako na safari kwa kusikiliza muziki au kuangalia TV kwenye basi, lakini vipi kwenye ndege  inakuwaje?

Jamaa mmoja Alex Simon mtalii kutoka Austria, alijikuta kwenye level za kistaa hivi au mtu fulani VIP kwenye ubora wake baada ya kujikuta akiwa ndio abiria pekeake ndani ya ndege ya abiria zaidi ya 100… alitoka zake  Manila kwenda Boracay ndani ya Ufilipino kwa ajili ya kutalii tu !!

Baada ya Simon kuingia kwenye ndege alianza kupiga stori na marubani baadae akaungana na wahudumu wawili wa ndege wakiendelea na stori mpaka alipotua

Cheki Video ya jamaa mwenyewe hii hapa mwanzo mpaka mwisho wa safari.