Tuesday, September 22

TAARIFA YA HABARI RASI FM RADIO SEPTEMBER 22.2015



KITAIFA:,
TANGA                                  
Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi. Samia Suluhu Hassan amevuna wanachama 272 Mkoani Tanga kutoka vyama mbalimbali vya upinzani baada ya wanachama wa vyama hivyo kujiunga rasmi na CCM.

Bi. Samia Suluhu ambaye ni mgombea mwenza wa Dk. John Pombe Magufuli amefanikiwa kuvunja ngome za wapinzani katika mikutano yake ya kampeni mjini Tanga baada ya wagombea udiwani watano wa ACT Wazalendo kujiunga na CCM pamoja na wanachama wengine 235 toka Tanga mjini kujiunga na CCM kwenye mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Usagara mkoani Tanga.
Akihutubia katika mkutano huo wa kampeni kunadi ilani ya CCM Tanga mjini uwanja wa Usagara, Bi. Samia Suluhu amewapokea wagombea udiwani watano kutoka ACT Wazalendo, wakiwemo Wilson Elia (wa Kata ya Duga), Gasper Maboko (Kata ya Nguvumali), Charles Luanda (Maweni) na Marry Scoty (Kata ya Tanga Sisi) pamoja na Sada Mbwambo (viti maalum).
Mbali na madiwani hao kukihama chama cha ACT, wanachama 235 kutoka ACT, CUF na Chadema wamejiunga na CCM kwenye mkutano huo wa Tanga mjini huku wengine 37 wakijiunga na CCM katika mkutano mwingine ulofanyika Jimbo la Muheza hivyo kutimiza wanachama 272 wapya kujiunga katika mikutano ya siku hiyo.
Akizungumza na wanaCCM na wananchi waliojitokeza mkutano wa Tanga Mjini, Bi. Suluhu amewaomba kuichagua CCM kurudi madarakani ili kuendeleza maendeleo iliyofikia katika maeneo mbalimbali, ikiwemo huduma za kijamii na miundombinu hasa ya barabara.
Bi. Samia amefanya mikutano minne mikubwa katika majimbo ya Mkinga, Pangani, Mheza na Tanga Mjini na mikutano midogo midongo sita alioifanya njiani akisimamishwa na wananchi wakitaka kumsikia alipokuwa akipita.
via Ippmedia --Edited by Denice Kazenzele
********************************************************************
MWANZA                            

Msajili wa vyama vya siasa nchini Mh.Jaji Francis Mutungi amewataka viongozi wa mathehebu ya dini,wamiliki wa vyombo vya habari na asasi za kiraia wasikubali kutumiwa na wanasiasa kuvuruga amani iliyodumu miaka 54 ya uhuru wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu 2015.
Wito huo umetolewa jijini Mwanza katika maadhimisho ya siku ya amani duniani ambapo kitaifa yamefanyika jijini humo na kuwahusisha, viongozi wa madhehebu ya dini, asasi za kiiraia, wasomi, walemavu, wamiliki wa vyombo vya habari na wandishi wa habari Mh.
Mkurugenzi mtendaji wa shirika la umoja wa mataifa linalojihusisha na utoaji elimu, sayansi na utamaduni kwa jamii UNESCO hapa nchini Bi.Zurmila Rodriguez amewataka watanzania kudumisha amani iliyopo miaka 54 ya uhuru hasa kwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu 2015 kwa kumuenzi baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere ambaye alipigania ukombzi wa nchi za Afrika na kuitangaza Tanzania kuwa kisiwa cha amani duniani.
Kwa upande wake kaimu mkuu wa mkoa wa Mwanza mchungaji Baraka Konisaga amesikitishwa na vurugu za wananchi kuchukua sheria mikononi kwa kuvunja gari la jeshi la polisi vioo ambapo naibu kamishina wa polisi ambaye ni kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Charles Mkubo ameuhakikishia umoja wa mataifa kuwa jeshi la polisi Tanzania limejipanga kikamilifu kuimalisha ulinzi wakati wa kampeni, siku ya kupiga kura na siku ya kutangaza matokeo.
Edited by Denice Kazenzele
 *******************************************************************
DAR ES SALAAM         
Wadau wa uzalishaji dawa ukanda wa Afrika Mashariki wanakutana jijini Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kujadili muongozo wa utumiaji wa dawa unaozingatia viwango vya kimataifa ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya mkutano wa kisekta uliokutanisha mawaziri wa masuala ya afya wa ukanda huo.

Ajenda kuu ya mkutano huo ni namna nchi zote tano za Afrika Mashariki zinavyoweza kuwa na matumizi sawa na viwango vinavyofanana vya dawa pamoja na kuhamasisha uwekezaji zaidi kwenye uzalishaji wa dawa.

Asilimia 80 ya dawa zinazotumika nchini huagizwa kutoka nje ya nchi, tena zikiwa na viwango tofauti, nyingine zikiwa chini ya viwango na nyingine zinazokubalika kwa kiwango cha kimataifa, kutokana na nchi zinapozalishwa dawa hizo na namna zinavyoingizwa.

Pamoja na tofauti za viwango, mkutano huo umejadili matumizi sahihi ya dawa ambayo yamekuwa na athari kubwa kwa watumiaji hususan kusababisha usugu wa dawa.

Miongoni mwa wadau wakuu kwenye eneo hilo, ni Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) ambayo imezungumzia mfumo huo mpya wa wazalishaji wa dawa unaoanza kutekelezwa kikanda na Jumuiya ya Afrika Mashariki na kudai utakuwa na tija kwa watumiaji na kuondoa usugu ambao ulijitokeza wakati wa matumizi ya dawa ambazo azina viwango.

Edited by Denice Kazenzele
 *****************************************************************
PWANI                               
Imeelezwa kuwa lishe bora ni muhimu kwa ustawi wa watoto kiafya na kielimu hivyo ni vyema kwa serikali kuingiza katika katiba ya nchi inayotambua moja kwa moja haki za watoto.
Kauli hiyo imetolewa na mgombea udiwani kata ya kisarawe kwa tiketi ya chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA katika mdahalo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe na kuwahusisha wagombea wa ngazi hiyo katika kata hiyo ili kuzungumzia ajenda za watoto kuzungumzwa katika jamii.
Akiinadi Ilani ya chama cha Demokrasia na Maendeleo, Baraka Musa anayegombea udiwani kata ya Kisarawe, amesema chama chake kinaamini kuwa lishe bora ni muhimu kwa ustawi wa watoto kiafya na kielimu na endapo kitaingia madarakani kitahakikisha kinawekeza kwenye kupata Katiba inayotambua na kuzitaja moja kwa moja haki za watoto.
Naye mgombea wa udiwani wa kata hiyo kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Abel Mudo amesema endapo chama chake kitapata ridhaa ya kuendelea kuongoza nchi kitawekeza zaidi katika shule na kuhakikisha zina walimu wa kutosha na kwamba serikali yake imetengeneza mazingira rafiki na kutoa zana kwa watoto wenye ulemavu.
Mgombea huyo ameahidi kufanya kazi pamoja na wadau mbalimbali ili kuhakikisha wanapunguza ukatili kwa watoto na kukabiliana na matatizo  ya mimba za utotoni sambamba na kutoa elimu bure kwa wanafunzi wa hadi kidato cha nne.
Edited by Denice Kazenzele
**************************************
KIMATAIFA:
OUAGADOUGOU                      

Jenerali Gilbert Diendere aliyefanya mapinduzi nchini Burkina Faso amesema yupo tayari kukabidhi serikali kwa utawala wa kiraia kama ilivyopendekezwa na wapatanishi.
Diendere ambaye alipindua serikali hiyo siku ya alhamisi wiki iliyopita amesema kuwa alifikia uamuzi huo kwa lengo la kile anachokiita kuepusha umwagaji mkubwa wa damu.
Burkina Demos

Kauli yake kukiri kukabidhi madaraka inakuja huku majeshi ya serikali yaki ukaribia mji mkuu wa Ouagadougou

Jeshi la Burkina Faso limeahidi kuwepo kwa hali ya Usalama kutokana na mapinduzi hayo,japo kuwa wameahidi kuto waangamiza waliofanya mapinduzi hayo iwapo tu watasalimisha silaha zao.

Hata hivyo kwa sasa Jeneral Diendere anadaiwa kujificha nyumbani kwa kiongozi wa kijadi Mogho Naaba.
bbcswahili/Re-Edited by Denice Kazenzele
 **************************************************************
 WASHINGTON                   
 
Scott Walker, ambaye ni miongoni mwa wagombea waliokuwa wakiwania kuteuliwa kugombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican amejiondoa katika kinyang'anyiro hicho.
Bwana Walker ambaye alikuwa gavana wa jimbo la Winscosin amesema amejitoa kwenye kampeni hizo ili kutoa nafasi kwa uteuzi wa mgombea muafaka atakayekabiliana na Donald Trump.
Mgombea huyo, ambaye alikuwa akiungwa mkono kwa wingi na wafuasi wa mrengo wa kulia, lakini hata hivyo katika kura ya maoni kiwango chake kilishuka baada ya kufanya vibaya katika midahalo.
Bbcswahili/Re-Edited by Denice Kazenzele
  ************************************************************
 MOGHADISHU                        SAA 06:00 MCHANA                         22.09.2015
picha hii haina uhusiano wa moja kwa moja na habari husika



Shambulizi lililotokea jana dhidi ya Ikulu ya Somalia mjini Mogadishu limesababisha vifo vya watu zaidi 9 na wengine 14 kujeruhiwa. 

Mabomu yaliyotegwa ndani ya gari yalilipuka usiku wa siku hiyo nje ya lango la Ikulu ya Somalia, na watu 9 wakiwemo askari wawili wa jeshi la serikali na wageni 3 waliuawa kwenye shambulizi hilo.
Siku hiyo maofisa wa serikali ya Somalia na baadhi ya wajumbe wa nchi nyingine walikuwa wakikutana kwenye Ikulu hiyo kujadili uchaguzi mkuu wa mwaka 2016.
Wakati mlipuko huo unapotokea, washiriki wengi wa mkutano huo walikuwa wameondoka, lakini walikuwepo maofisa wachache waliobaki ambao ni kati ya waliouawa na kujeruhiwa.
Kundi la Al-Shabaab limetangaza kufanya shambulizi hilo dhidi ya maofisa wa serikali ya Somalia. 

Cri/Re-Edited by Denice Kazenzele

No comments: