Saturday, November 26

FIDEL CASTRO ALIYEKUWA RAIS WA CUBA HATUNAE TENA...R.I.P



Rais wa zamani wa Cuba na kiongozi wa mapinduzi ya kikomunisti, Fidel Castro amefariki akiwa na umri wa miaka 90, mdogo wake Raul ametangaza.

Thursday, November 17

JK AWATUNUKU DIGRII WAHITIMU 1,179 CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU DUCE

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm), Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete (wa pili kulia) akimkabidhi zawadi mwanafunzi bora wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (Duce), Haji Mohamed wakati wa Mahafali ya Tisa ya chuo hicho leo. Jumla ya wanafunzi 1,179 walihitimu na kutunukiwa digrii za awali. 

SERIKALI YABARIKI UZINDUZI WA TELEVISHENI YA KIDIGITALI KUTOKA STARTIMES


Serikali kupitia Wizara ya Ujezi Uchukuzi na Mawasilano imebariki uzinduzi wa televisheni mpya ya kidigitali kutoka kampuni ya Startimes Tanzania. 

Wednesday, November 16

KIWANDA CHA KUTENGEZA VIROBA FEKI CHAKAMATWA.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla, akiwa ameongzana na timu ya Serikali yenye wataalamu na wanausalama wameendesha operesheni kali ya kusaka viroba feki na pombe nyingine haramu katika maeneo ya Jiji la Dar es Salaam  na kufanikiwa kukama shehena kubwa ya bidhaa hizo feki na haramu kwenye maeneo  hayo.

Monday, November 14

“SEEING THE UN DELIVERING AS ONE IN DAR ES SALAAM, DODOMA AND KIGOMA”


The Nordic countries (Sweden, Norway, Denmark, Finland and Iceland) are key donors and partners of the United Nations system globally, regionally and at country level. In order to strengthen their collaboration with the United Nations in support of the Global Goals, and strategic development priorities of the Government of Tanzania, officials representing the five Nordic countries will be in the country during 14 -18 November, 2016.

AZAM FC YASAKA NA KUANDAA VIPAJI VIPYA


TanzaniaImage copyrightGOOGLE
Image captionVijana wakipepetana kuwania nafasi ya malezi ya vipaji maalum

Vijana saba wenye umri chini ya miaka 17, wamepenya kwenye majaribio ya wazi ya mwisho katika mkoa wa Dar es Salaam, yaliyoendeshwa na Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC mwishoni mwa juma.

DONALD TRUMP AFANYA UTEUZI WA AWALI.



MarekaniImage copyrightAFP
Image captionReince Priebus alionekana na Donald Trump usiku wa siku ya uchaguzi

Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, amemteua mwenyekiti wa kamati ya taifa ya chama cha Republican, Reince Priebus, kutumika kama mkuu wa wafanyakazi.

TAIFA STARS YABAMIZWA 3-0 NA WARRIORS YA ZIMBABWE ,NYOTA WA KV OOSTENDE YA UBELGIJI AMUONESHA SAMATTA MAVITU

samata1
Mshambuliaji wa Taifa Stars, Elius Maguri akichuana na beki wa Zimbabwe, Hadebe Teenage katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika Uwanja wa Taifa wa Zimbabwe leo. Tanzania ilifungwa mabao 3-0.

Sunday, October 9

HILI LA CHRISS BROWN KUVUNJA SIMU YA SHABIKI KENYA NI KWELI AU NI KAWAIDA YA MAJIRANI KUTAFUTA KIKI?


Muimbaji mashuhuri wa Marekani mtindo wa Hip Hop Chris Brown, yupo Kenya kwa tamasha la muziki mjini Mombasa eneo la pwani.

US 'REVIEWING' SUPPORT FOR SAUDI CAMPAIGN IN YEMEN FOLLOWING FUNERAL MASSACRE

Jemen Luftangriffe in Sanaa mit Dutzenden Toten und Verletzten (Getty Images/AFP/M. Huwais)

Washington has ordered an "immediate review" of its support for the Saudi-led coalition in Yemen after a strike on a funeral in the capital killed more than 140 people. The UN is pushing for an independent probe.

HIVI NDIVYO CHEGE ALIVYOSHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA KATIKA HOSPITALI YA TEMEKE


PICHA: Chege alivyosherehekea siku yake ya kuzaliwa katika Hospitali ya Temeke





Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la Wanaume Family, Chege Chigunda, ameadhimisha siku yake ya kuzaliwa kwa kutembelea hospitali ya Rufaa ya Temeke na kugawa zawadi mbalimbali katika wodi ya Watoto waliolazwa hapo kutokana na matatizo mbalimbali.

HUYU HAPA ASKOFU MPYA WA KKKT DAYOSISI YA IRINGA

Askofu  wa kanisa la  kiinjili la  Kilutheri  Tanzania (KKKT)  dayosisi ya  Iringa Dkt  Owdenburg Mdegela katikati  akiwatambulisha  mbele ya waumini wa kanisa  kuu  askofu  mteule wa dayosisi  hiyo mchungaji  Blaston  Gavile (wa  pili kushoto)   na mkewe  pamoja na msaidizi wa askofu huyo mchungaji Himid Saga  (wa pili  kulia)  na mkewe

SHEREHE ZA MWENGE WA UHURU ZILIVYOFANA WILAYANI KISHAPU


Mwenge wa Uhuru umewasili na kupokelewa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ukitokea Manispaa ya Shinyanga mkoani Shinyanga.

EALA SITTING FOR ZANZIBAR NEXT WEEK


secEAC Secretary General Amb. Liberat Mfumukeko
……………………………………………………………………..
The East African Legislative Assembly (EALA) shall hold its Sitting in Zanzibar, Tanzania, next week. The Plenary which takes place from Monday, October 10th, 2016 to Friday, October 21st, 2016, is the Second Meeting of the Fifth Session of the Third Assembly.
The Assembly is to be presided over by the Speaker, Rt. Hon. Daniel F. Kidega. Top on the agenda during the two-week period is the Special Sitting on Tuesday, October 11th, 2016, which is expected to be addressed by the President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, H.E. Dr. Ali Mohamed Shein.
This is the first time the 3rd Assembly is meeting in Zanzibar as part of its rotational principle.   The 2nd Assembly on its part held a Sitting in Zanzibar in December 2007.
The Assembly is expected to dispense with three key Bills, the EAC Trafficking in Persons Bill 2016, the EAC Polythene Materials Control Bill 2016 and the EAC Gender Equality and Development Bill 2016.
The EAC Counter-Trafficking in Persons Bill, 2016, seeks to provide a legal framework, develop common measures, strategies and programmes to the prevention of trafficking in persons and the perpetrators of such actions. The Bill is being debated at a time when the region and the globe are reeling from major effects of counter-trafficking in persons.  
The Bill is to further develop partnerships for co-operation in counter trafficking in persons and provision of protection mechanisms and services for persons.  At the Sitting in Dar es Salaam in March 2016, the Assembly committed the crucial Bill to the Committee stage.
The EAC Polythene Materials Control Bill, 2016 moved by Hon. Patricia Hajabakiga, aims at providing a legal framework for the preservation of a clean and healthy environment through the prohibition of manufacturing, sale, importation and use of polythene materials.  The Bill was re-introduced during the Sitting held in August 2016 in Arusha, Tanzania.
The EAC Gender Equality and Development Bill 2016 on its part, sets out to make provision for gender equality, protection and development in the Community.
According to the mover, Hon. Nancy Abisai, the Bill seeks to consolidate and harmonise the various commitments on gender equality that have been made at regional, continental and international levels in the context of the EAC.
The EAC Partner States appreciate the importance of women and men’s participation in the integration process of the EAC. At the same time, the Partner States are signatories to and should adhere to the instruments and take cognizance of emerging threats such as feminization of poverty, globalization, and gender based violence – all of which impact negatively on citizens.
The House shall also be furnished by a number of reports. They include Reports of the Committee on Communication, Trade and Investments, the Committee on Regional Affairs and Conflict Resolution and the Committee on Legal, Rules and Privileges. The Committee on Agriculture, Tourism and Natural Resources and the General Purpose Committee shall also be tabling their reports.
EALA Sittings are held under the principle of rotation in line with Article 55 of the EAC Treaty. EALA meets at least once in every year at its headquarter in Arusha, Tanzania.

SABABU KIFO CHA MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WANAWAKE TANZANIA (UWT) DODOMA


Mashuhuda  wa ajali iliyosababisha kifo cha Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, Salome Kiwaya wamesema alikufa kutokana na kushindwa kupewa msaada kwa haraka.

Walisema baada ya ajali walisikia sauti za watu wakilia kuomba msaada lakini ilichukua muda wa sasa tatu ndipo walipopata msaada wa kuokolewa kutokana na ukosefu wa vifaa vya uokoaji.

Juzi katika eneo la Emmaus mkoani hapa ilitokea ajali ya gari la Toyota Noah na lori ambayo ilichukua maisha ya Mwenyekiti huyo na watu wengine watatu kujeruhiwa. 

Mmoja wa mashuhuda hao Amri Juma alisema alisikia sauti za wanawake wakiomba msaada ili waweze kuokolewa.

“Ni jambo la kusikitisha kuona zaidi ya saa tatu hakuna vifaa vya uokoaji vilivyokuwa vimefika kwa ajili ya uokoaji, ajali ilitokea saa nane mchana lakini mpaka saa 11 jioni ndio watu wanakuja kutolewa.

‘’‘Breakdown moja ilipofika ilishindwa kunyanyua lori, ilipofika ya pili ilishindwa, hali inayoonesha kuna uhaba wa vifaa hivyo mamlaka husika zijipange kuwa na vifaa vya uokoaji."

 Juma alisema Dodoma imeanza kuandaliwa kuwa makao makuu ya nchi hivyo wakati umefika wa kuanza kujengewa uwezo wa kuwa na vifaa vya kisasa vya uokoaji. 

Katibu wa UWT Mkoa wa Dodoma, Kaundime Kasase, akizungumzia kifo hicho alisema;

“imeniuma sana na bado inaniuma, sina hata la kusema kwani nimefanya naye kazi kwa ukaribu, alikuwa mtu anayependa viongozi wake wote."

Mtoto aliyekuwa ndani ya gari hilo, Dearest Mabuba (8) alisema;“Tulikuwa tumetoka kwenye birthday (siku ya kuzaliwa) yangu ndipo gari likapata ajali, mama yangu Annastazia Amandus ambaye alikuwa akiendesha gari hilo akaumia kichwani na dada akachanika kwenye kiwiko,” alisema.

Meya wa Manispaa ya Dodoma, Jaffari Mwanyemba alisema wamempoteza mtu muhimu.

“Alikuwa akijichanganya kila mahali, tumepoteza mtu muhimu tuige mazuri yake”. 

Mbunge wa Viti Maalumu na Mwenyekiti mstaafu wa UWT Mkoa wa Dodoma, Fatma Tawfiq alisema;

“Mwenyezi Mungu ndiye alikuwa akifahamu siri hii. “Ni jambo la kushtukiza sana tumuombee Mungu amuweke mahali pema peponi,”alisema.

Hata hivyo kwa upande wake, Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Dodoma, Marson Mwakyoma alisema walifika eneo la tukio dakika 10 baada ya ajali hiyo kutokea.

“Si lazima askari avae sare tulifika mapema na vikosi vingine vya uokoaji vilikuja kwa wakati, nadhani kitu muhimu kinachotakiwa kufanyika ni kuimarisha vifaa vya uokoaji,” alisema.

Saturday, October 8

Body Parts You Didn’t Know Had Names! 0

Glabella. The glabella is the space between the eyebrows. A glabellar reflex is a primitive reflex found in patients with Parkinson’s disease. When repeatedly tapped on the forehead, they blink continuously. Normal people do not.

HIZI HAPA KURASA ZA MBELE NA NYUMA ZA MAGAZETI YA LEO OKT 8/2016

ZSSF TENDER : PROVISION OF CLEANING SERVICES AT ZSSF PREMISES, ZANZIBAR

ZANZIBAR SOCIAL SECURITY FUND
                                                                P.OBOX 2716,
                                                KILIMANI MNARA WA MBAO,
                                                                  ZANZIBAR

Tender No. ZSSF/2016/2017/NC/01
For
Provision of Cleaning Services at ZSSF Premises, Zanzibar

 

Friday, October 7

KUHUSU HALI YA HEWA KWA LEO NA KESHO TANZANIA

MINISTRY OF WORKS, TRANSPORT AND COMMUNICATION

TANZANIA METEOROLOGICAL AGENCY-TMA

P.O.BOX 3056, DAR ES SALAAM
Tel / fax. 2460772.
LAKE VICTORIA ZONE.
WEATHER FORECAST FOR THE NEXT 24 HOURS STARTING AT 9.00PM, 07/10/2016
This forecast is for Mwanza, Kagera, Mara and Shinyanga regions.

DR.MAGUFULI ATISHIA KUMFUTA KAZI MTOTO WA DADA YAKE KWA KISA HIKI.................


Rais Dkt John Pombe Magufuli ametishia kufukuza kazi mtoto wa dada yake kutokana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kutopeleka umeme katika kiwanda kipya cha kusindika matunda cha Bakhresa.

CHAMA CHA WANANCHI {CUF} HATARINI KUFUTWA


Mgogoro unaoiandama CUF huenda ukailetea balaa zaidi, baada ya kuwapo kwa taarifa kuwa huenda ikafutwa kama itazidi kukomalia msimamo ilionao wa kutotaka ushauri.

RUSSIA YAIONYA VIKALI MAREKANI, YASEMA HAIWEZI KUKABILIANA NA S300, S400

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Russia, Igor Konashenkov amesema kuwa, shambulio lolote la kombora au la anga litakalolenga maeneo ya jeshi la serikali ya Syria, litakuwa linahatarisha majeshi ya Russia na Syria kwa pamoja.
Konashenkov ameitaka Marekani kuzingatia kwa umakini matokeo mabaya yatakayotokana na hatua yake ya kushambulia maeneo ya jeshi la Syria.
Msemaji wa Wizara ya Ulinzi nchini Russia, Igor Konashenkov.
Ameingeza kuwa, baada ya hujuma ya anga iliyofanywa na ndege za kivita za Marekani tarehe 17 Septemba dhidi ya jeshi la  Syria, Moscow ilichukua hatua za lazima za kuzuia kujikariri tukio kama hilo dhidi ya jeshi lake nchini Syria.

WAFANYABIASHARA WA DRC WAIPONGEZA SERIKALI YA TANZANIA.

k1
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Congo (DRC) nchini Tanzania Bw. Sumail Edward (kulia) akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari kuhusu uamuzi wa wafanyabiashara wa Congo kutumia Bandari ya Dar es Salaam baada ya Serikali kuondoa vikwazo, kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari  Bw. Tiganya Vincent.
k2
Baadhi ya waandishi wa habari wakimfuatilia kwa makini Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Congo (DRC) nchini Tanzania Bw. Sumail Edward (mwenye suti) wakati alipokuwa akielezea kuridhika na uamuzi wa Serikali ya Tanzania kuondoa vikwazo katika Bandari ya Dar es Salaam na kupelekea wafanyabiashara wa Congo (DRC) kuendelea kuitumia bandari hiyo.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MADUDU MAMLAKA YA USTAWISHAJI MAKAO MAKUU DODOMA (CDA)


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Bunge), Bw. Uledi Mussa afuatilie malipo ya kiwanja kilichouzwa na CDA kwa sh. milioni 240 lakini fedha iliyoingia ofisini ni sh. milioni 6 tu.

LIGI YA WANAWAKE KUANZA KUTIMUA VUMBI NOVEMBA MOSI, TIMU 12 KUSHIRIKI


Timu 12 zinatarajiwa kushiriki Ligi ya Taifa ya Wanawake inayotarajiwa kuanza Novemba mosi, mwaka huu kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Maendeleo ya Soka la Wanawake na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), zilizoridhia tarehe hiyo.

COLOMBIAN PRESIDENT JUAN MANUEL SANTOS WINS NOBEL PEACE PRIZE


Colombian President Juan Manuel Santos was awarded the Nobel Peace Prize for his efforts to bring the country’s 52-year old conflict with the FARC rebels to an end. 
Santos had managed to secure a peace deal with the FARC rebels, although it was voted down in a referendum less than a week ago.

Thursday, October 6

RIDHIWANI ASAIDIA MAGODORO 50 MORETO BAADA YA BWENI KUUNGUA

more
BWENI la wanafunzi wasichana katika shule ya sekondari ya Moreto iliyopo tarafa ya Msoga wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, baada ya kuungua kwa moto na kusababisha mali zote za wanafunzi hao kuteketea kwa moto. (Picha na Mwamvua Mwinyi)
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
MBUNGE wa jimbo la Chalinze, mkoani Pwani, Ridhiwani Kikwete, ametoa magodoro 50, yenye thamani ya sh.mil 2.225 kwa wanafunzi wa kike wa shule ya sekondari Moreto, waliounguliwa na bweni lao na kusababisha mali zote kuteketea kwa moto.
Wanafunzi hao wapatao196, katika shule hiyo iliyopo kata ya Lugoba tarafa ya Msoga, wilaya ya Bagamoyo, wamenusurika kifo baada ya bweni hilo kuteketea kwa moto siku ya october 5.
Moto huo umeteketeza mali zote zilizokuwemo ambazo hadi sasa hazijajulikana thamani yake.
Kufuatia kutokea kwa tukio hilo, Ridhiwani alifika shuleni hapo kutembelea na kutoa pole kwa kutokea janga hilo.
Alisema wakumshukuru ni mungu kwani pamoja na kutokea kwa hasara ya kuteketea kwa mali lakini hakuna madhara kwa wanafunzi yaliyotokea.
Ridhiwani aliwapa pole walimu na wanafunzi kijumla na kuwaomba wadau wengine kujitokeza kwenda kusaidia pale watakapojaaliwa.
Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Moreto, Justine Lyamuya alielezea kuwa, tukio hilo limetokea October 5,majira ya asubuhi ambapo walianza kuona moshi mzito katika bweni mojawapo wanaloishi wasichana wa shule hiyo.
Alisema wakati moto huo unazuka wanafunzi hao walikuwa kwenye masomo yao darasani.
“Tulifuatilia na kukuta moto umeshashika kwenye bweni hilo na jitihada za kuuzima zilishindikana”alisema mwalimu Lyamuya.
Lyamuya alisema mali zote za wanafunzi wanaolala kwenye bweni hilo zimeteketea kwa moto hivyo kwa sasa wanafanya tathmini kujua gharama zilizopotea.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini chanzo cha moto.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani, Boniventure Mushongi, alielezea kuwa mazingira ya jengo hilo ni yenye kutumia nishati ya solar power hivyo ni lazima kufanya uchunguzi wa kina kujua kiini cha kuzuka kwa moto huo.
Alisema bweni hilo linakadiriwa kuwa na wanafunzi 196.
Kamanda Mushongi alisema thamani za mali za wanafunzi katika moto huo bado hazijafahamika.

Sunday, May 22

YANGA SC YAMKUNA RAIS WA FIFA GIANNI INFANTINO


Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), Gianni Infantino, ameipongeza timu ya soka Young Africans ya Dar es Salaam, kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2015/16.

PROF: MUHONGO: MIKATABA YA TANESCO NA IPTL HAINA FAIDA KWA TAIFA



Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amesema mikataba yote ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni za kufua umeme siyo mizuri na haina manufaa yoyote kwa Taifa.

Saturday, April 30

MKURUGENZI WA IDARA YA MAAFA NCHINI ATEMBELEA MAENEO YALIYOATHIRIKA KWA MAFURIKO.

Mbunge wa jimbo la Vunjo ,James Mbatia akizungumza jambo na Mkurugenzi wa idara ya Maafa nchini Brigedia Jenerali Mbazi Msuya wakati wakitembelea kijiji cha Mandaka Mnono kujionea athari ya mafuriko,katikati ni Mbunge wa viti Maalum (Chadema) mkoa wa Kilimanjaro Lucy Owenya.