Friday, November 20

KWA HEWA LEO..Magazetini Tanzania November 20 2015 kwenye kurasa za mbele na za nyuma.....


DSC02508 DSC02509 DSC02510 DSC02511 DSC02512 DSC02513 DSC02514 DSC02515 DSC02516 DSC02517 DSC02518 DSC02519 DSC02520 DSC02521 DSC02522 DSC02523 DSC02524 DSC02525 DSC02526 DSC02527 DSC02528 DSC02529 DSC02530 DSC02531 DSC02533 DSC02534 DSC02535 DSC02536 DSC02537 DSC02538 DSC02539 DSC02540 DSC02541 DSC02542 DSC02543 DSC02544 DSC02545 DSC02546 DSC02547 DSC02548 DSC02549 DSC02550 DSC02551 DSC02552

MKALI WA ACTION MOVIE....Pichaz 8 za mkali wa movie kutoka Hollywood Van Damme alivyotembelea mazoezi ya Man City.....


Staa wa movie kutoka Hollywood Jean-Claude Van Damme mkali ambaye amewahi kutamba na movie kadhaa November 19 alipata nafasi ya kutembelea mazoezi ya klabu ya Manchester City. Staa huyo wa Hollywood yupo jijini Manchester kwa ajili ya shughuli ya ‘black-tie dinner’ ambapo atapata nafasi ya kuoneshwa kwa movie zake.
2E9B924D00000578-3325905-image-a-23_1447960227983
Jean-Claude Van Damme na Vincent Kompany
Jean-Claude Van Damme ambaye ana umri wa miaka 55 alivyotembelea mazoezi ya Man City mastaa wa klabu hiyo hawakuacha kuchukua kumbukumbu zao kwa kupiga picha na staa huyo, wachezaji wa Man City kama Yaya Toure, Vincent KompanyKevin De Bruyne, Sergio Aguero pamoja na kocha wao Manuel Pellegrini hawakusita kupiga picha na Van Damme.
2E9B927C00000578-3325905-The_80s_action_movie_hero_poses_for_a_picture_with_Belgian_compa-m-11_1447959922108
Jean-Claude Van Damme na Vincent Kompany
Mkali huyo wa movie duniani ambaye kwa miaka ya karibuni ametamba katika tangazo la bia, amewahi kutamba katika movie za mapigano zikiwemo BloodsportHard Target na Universal Soldier. Hizi ni baadhi ya pichaz zake alivyotembelea Man City.
2E9B970600000578-3325905-image-a-21_1447960121031
2E9B945600000578-3325905-image-a-20_1447960070642
Jean-Claude Van Damme na golikipa wa Man City Joe Hart
2E9B971E00000578-3325905-image-a-5_1447959538287
Sergio Aguero na Jean-Claude Van Damme
2E9B934600000578-3325905-image-a-8_1447959792555
Jean-Claude Van Damme Kevin De Bruyne
2E9B977000000578-3325905-image-a-10_1447959881627
Kocha wa Man City Manuel Pellegrini akiwa na Jean-Claude Van Damme
0064DDFD00000258-3325905-image-a-17_1447960042452
Universal Soldier hii ni movie aliyotamba nayo miaka ya 1990 aliyoicheza Jean-Claude Van Damme alicheza pamoja na Dolph Lundgren

Thursday, November 19

Twende Paris...Ufaransa yaonya kuhusu shambulio la sumu....

MSHUHUDIE KILICHOMTOKEA...Mchungaji kawalisha waumini nyoka na nguo za ndani!!!..


Hizi stori kutoka kwa viongozi wa nyumba za ibada kuwa na matendo yanayoibua maswali mengi sio ngeni masikioni mwetu, nimeinasa nyingine toka South Africa, Mchungaji kawalisha Waumini wake nyoka pamoja na nguo za ndani..
Penuel-Mnguni-of-End-Times-Disciples-Ministries-1
Mchungaji huyo Penuel Mnguni ambaye ni Kiongozi wa Kanisa la End Times Disciples Ministries lililopo katika Mji wa Soshanguve ulioko Pretoria South Africa, alijikuta akiishia mikononi mwa watu wenye hasira na matendo yake, huku Kanisa lake likiteketea baada ya kuchomwa moto na watu haohao !!
Penuel-Mnguni-of-End-Times-Disciples-Ministries-2
Taarifa zilienea mitaani kuhusu huduma zake, alikuwa akiwalazimisha waumini wake kula nyoka pamoja na nguo za ndani kama sehemu ya huduma za Kanisa lake kwa Waumini… watu wa eneo hilo waliwavamia na kumkamata Mchungaji huyo, Kanisa likaishia kuchomwa moto, ambapo baada ya muda kidogo ilibidi Polisi waingilie kati kumuokoa.

HUYU HAPA NDIYO WAZIRI MKUU WA TANZANIA KUTOKA BUNGENI..2015....

BREAKING NEWS: Mh. Kassim Majaliwa Mbunge wa Ruangwa amependekezwa na Rais John Magufuli kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Waziri Mkuu aliyependekezwa Mh. Kassim Majaliwa ni mbunge kupitia jimbo la Ruangwa na ana umri wa miaka 54.

TAIFA STARS..Kichapo cha Bao 7-0 kwa Taifa Stars dhidi ya Algeria kimemvunjia rekodi hii Mkwasa …

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars November 17 ilicheza mchezo wake wa pili wa marudiano ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2018 Urusi dhidi ya Algeria Blida katika uwanja wa Mustapha Tchaker  na kukubali kipigo cha magoli 7-0,  idadi ya magoli ambayo iliifanya Tanzania kuingia katika headlines ya ya kufungwa idadi kubwa ya magoli.
November 18 kocha wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa ameongelea namna alivyokipokea kipigo hicho na kufanya kiweke historia kwake kwani kwa miaka yake 25 katika soka hakuwahi kuweka rekodi ya kupokea kipigo cha magoli mengi kiasi hicho kitu ambacho hakikuwaumiza watanzania hata yeye.
DSC_0041
“Kiukweli hata mimi ilinishangaza kidogo na tulizidiwa umeona uwezo wa mchezaji wao Yacine Brahimi uwezo wake ni mkubwa kikosi chao kilibadilika ila uwanja pia ulikuwa tatizo ulikuwa unateleza hata goli la kwanza tulilofungwa lilitokana na hivyo, kufungwa goli 7 sijawahi kiukweli katika miaka 25 yangu katika soka” >>> Boniface Mkwasa

SOMA HAPA..Stori za Magazetini ya leo Tanzania November 19 2015 kwenye kurasa za mbele na za nyuma...

Wednesday, November 18

Rapa Mkali Toka Kitambo..Snoop Dogg aponda vikali orodha ya Billboard ya rappers wakali wa muda wote....

Snoop-Dog-Main
Rapa mkongwe duniani Snoop Dog ameponda vikali orodha ya rapa wakali zaidi wa muda wote iliyotolewa na tovuti ya Billboard wiki iliyopita.
Majina kwenye orodha hii yalikuwa pamoja na Biggie, Jay Z, Eminem, Rakim, Nas, Andre 3000, Lauryn Hill, Ghostface Killah, Kendrick Lamar na Lil Wayne.
Snoop Dogg amekasirishwa kuwa Tupac hakutajwa kwenye orodha hii. Haya ndio maneno yake kwenye instagram >>This is so disrespectful. !!Whoever did this list need a swift kick in the Ass. No. Tupac. Come on cuz ?. Jus my opinion.
billboard

AGEUKA KIVUTIO ALGERIA...ANGALIA HUYU MWARABU ALIVYOKUWA AKIMUANGALIA SAMATTA....

WAKATI WACHEZAJI WA TAIFA STARS WAKITEMBEA KATIKA MITAA YA BILDA, MBWANA SAMATTA ALIENDELEA KUWA KIVUTIO NA MASHABIKI WALIKUWA WAKITAMANI ANGALAU KUPIGA NAYE PICHA. ANGALIA SHABIKI HUYO ALIVYOKUWA AKIZUBAA UTAFIKIRI KAMUONA SAMUEL ETO'O.




HATIMAYE AIBUKIA KINONDONI....KMC FC YAANZA MAZUNGUMZO NA SELEMANI MATOLA....


Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, amethibitisha kuwa kwenye mazungumzo na Klabu ya Manispaa ya Kinondoni (KMC FC) inayoshiriki Ligi Darala la Kwanza, lakini hofu imetanda klabuni hapo, kwani imebainika haziivi na kocha wa timu hiyo, Amri Said ‘Jap Stam’ ambaye pia aliwahi kuwa kwenye benchi la Simba msimu wa 2010.

Matola ambaye aliachana na Simba wiki iliyopita kwa kile alichobainisha ni kutokuwa na maelewano mazuri na kocha mkuu, Dylan Kerr, amesema amefanya mazungumzo na uongozi wa klabu ya KMC FC, lakini bado hawajafikia muafaka.

“Wao walinifuata tukazungumza kiutendaji lakini hakukuwa na muafaka katika mazungumzo yetu. Kama tutamalizana vizuri taarifa zitatolewa tu na siyo jambo la kuficha,” alisema Matola.
Hata hivyo, kuonyesha kuwa uhusiano wake na Matola siyo mzuri, Stam alipoulizwa kuhusu Matola kukaribia kujiunga na timu hiyo, alisema:

“Sijaambiwa chochote kuhusu kumtaka Matola ingawa taarifa hizo ninazo, kuwa wanataka tusaidiane kuhakikisha tunaipandisha timu ligi kuu. Nafikiri hilo siyo jukumu lao ni jukumu la kocha mkuu, hivyo walikuwa na kila sababu ya kunifuata kuniuliza kuhusu mtu sahihi katika kusaidiana katika harakati hizi.

“Timu inafanya vema na dhamira yangu kuu ni kuipandisha ligi kuu, hivyo kama ni masuala haya, wanataka kutibua hali ya mambo. Mimi ndiye ninatakiwa kumtafuta msaidizi wangu na siyo mtu yeyote, maana mimi ndiye kocha mkuu,” alifunguka kocha huyo aliyewahi pia kuzifundisha Mwadui na Ndanda.

SIKIA KAULI YA NAHODHA HUYU...ZLATAN KIBURI, JEURI! ATANGAZA KULISTAAFISHA SOKA TAIFA LOTE LA DENMARK......


Nahodha wa Sweden, Zlatan Ibrahimovich amefunga moja kati ya mabao mawili yaliyoiwezesha Sweden kusonga mbele katika kuwania kucheza Kombe la Dunia baada ya kuing'oa Denmark.

Awali, Denmark walitamba kumstaafisha soka Zlatan, lakini baada ya sare ya 2-2, Sweden imesonga kwa jumla ya mabao 4-3 na Zlatan amesema: "Sasa taifa lao lote, nimelistaafisha soka."

Denmark na Sweden ni majirani ambao wana ushindani wa hali ya juu.

Denmark (4-2-3-1): Schmeichel 6.5; Jocobsen 6, Kjaer 5, Agger 6, Durmisi 5.5 (Vestergaard 83); Hojbjerg 6, Delaney 6.5 (Krohn-Dehli 45, 6); Poulsen 6.5, Eriksen 6, Jorgensen 6; Bendtner 5
Subs not used: Andersen, Wass, Kvist Jorgensen, Braithwaite, Christensen, Falk Jensen, Simon Poulsen, Jakob Poulsen, Rasmussen, Lossl.
Booked: Durmisi, Poulsen, Hojbjerg 
Sweden (4-4-2): Isaksson 6.5; Lustig 6.5, Johansson 6, Granqvist 5.5, Bengtsson 5 (Olsson 86); Larsson 6.5 (Hiljemark 81), Lewicki 6.5, Kallstrom 6 (Svensson 69), Forsberg 6; Berg 6, Ibrahimovic 8.5
Subs not used: Olsen, Helander, Guidetti, Kujovic, Milosevic, Toivonen, Durmaz, Zengin, Carlgren.
Booked: Bengtsson, Larsson 
Referee: Martin Atkinson (England) 6.5







KOCHA WA YANGA..PLUIJM ALIA CHALENJI KUHARIBU PROGRAMU NA KAMBI NZIMA.....


Yanga imeshindwa kuingia kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara kutokana na michuano ya Kombe la Chalenji iliyopangwa kuanza Novemba 20 jijini Addis Ababa, Ethiopia.


Yanga hivi sasa inaendelea na maandalizi ya ligi kuu chini ya Kocha Mkuu, Mholanzi, Hans van Der Pluijm na Juma Mwambusi wakati ligi hiyo ikisimama.

Pluijm amesema ni ngumu kuifuata programu aliyoipanga wakati ligi kuu ikisimama kutokana na nusu ya wachezaji kuwepo vikosi vya timu zao za taifa.

Pluijm alisema, katika ripoti yake aliomba mechi tano za kirafiki za kimataifa pamoja na kambi ya pamoja ya kujiandaa na ligi hiyo katika kuhakikisha wanautetea ubingwa wao.

“Timu inaendelea na mazoezi yake ya pamoja ikiwa na mchanganyiko wa wachezaji wa U20 baada ya nusu ya wachezaji wa timu kubwa kuwepo kwenye timu zao za taifa.

“Hivyo hivi sasa siwezi nikafanya chochote ikiwemo kucheza mechi za kirafiki za kimataifa, pamoja na kambi ya kujiandaa na ligi kuu iliyosimama hadi pale wachezaji wote watakaporejea kujiunga na wenzao,” alisema Pluijm.

ETI LAZIMA WAONDOKE...BOMOA BOMOA MWENGE JIJINI DAR ES SALAAM LEO.......

Tingatinga likiendelea na kazi ya kubomoa nyumba na vibanda vya biashara vilivyojengwa isivyo halali katika maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam leo huku baadhi ya wananchi wakijaribu kunusuru baadhi ya mali.
Wananchi wakijaribu kuokoa mali zao baada ya maduka na nyumba kadhaa zilizojengwa isivyohalali kuvunjwa katika maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam

Polisi Marekani yawatia nguvuni wanaharakati weusi...


Polisi Marekani yawatia nguvuni wanaharakati weusi
Maafisa wa polisi nchini Marekani wamewatia mbaroni zaidi ya wanaharakati 50 waliokuwa wakishiriki maadamano katika jimbo la Minnesota. Mamia ya wanaharakati hao wamefanya maandamano ya kukashifu dhulma wanazopitia watu weusi nchini humo.
Chini ya kaulimbiu “Black Lives Matter” waandamanaji hao walifunga barabara kuu ya Minnesota huku wakiwa wamebeba mabango na maberamu yaliyokuwa na jumbe za kulaani ubaguzi wa rangi. 
Maandamano hayo yalinuia kuishinikiza polisi ya Minnesota kufafanua sababu za kuuawa kijana wa miaka 24 kwa jina Jamar Clack, mikononi mwa polisi katika jimbo hilo Jumapili iliyopita.