Friday, November 20
MKALI WA ACTION MOVIE....Pichaz 8 za mkali wa movie kutoka Hollywood Van Damme alivyotembelea mazoezi ya Man City.....
Staa wa movie kutoka Hollywood Jean-Claude Van Damme mkali ambaye amewahi kutamba na movie kadhaa November 19 alipata nafasi ya kutembelea mazoezi ya klabu ya Manchester City. Staa huyo wa Hollywood yupo jijini Manchester kwa ajili ya shughuli ya ‘black-tie dinner’ ambapo atapata nafasi ya kuoneshwa kwa movie zake.
Jean-Claude Van Damme ambaye ana umri wa miaka 55 alivyotembelea mazoezi ya Man City mastaa wa klabu hiyo hawakuacha kuchukua kumbukumbu zao kwa kupiga picha na staa huyo, wachezaji wa Man City kama Yaya Toure, Vincent Kompany, Kevin De Bruyne, Sergio Aguero pamoja na kocha wao Manuel Pellegrini hawakusita kupiga picha na Van Damme.
Mkali huyo wa movie duniani ambaye kwa
miaka ya karibuni ametamba katika tangazo la bia, amewahi kutamba katika
movie za mapigano zikiwemo Bloodsport, Hard Target na Universal Soldier. Hizi ni baadhi ya pichaz zake alivyotembelea Man City.
Thursday, November 19
MSHUHUDIE KILICHOMTOKEA...Mchungaji kawalisha waumini nyoka na nguo za ndani!!!..
Hizi stori kutoka kwa viongozi wa nyumba
za ibada kuwa na matendo yanayoibua maswali mengi sio ngeni masikioni
mwetu, nimeinasa nyingine toka South Africa, Mchungaji kawalisha Waumini
wake nyoka pamoja na nguo za ndani..
Mchungaji huyo Penuel Mnguni ambaye ni Kiongozi wa Kanisa la End Times Disciples Ministries lililopo katika Mji wa Soshanguve ulioko Pretoria South Africa,
alijikuta akiishia mikononi mwa watu wenye hasira na matendo yake, huku
Kanisa lake likiteketea baada ya kuchomwa moto na watu haohao !!
Taarifa zilienea mitaani kuhusu huduma
zake, alikuwa akiwalazimisha waumini wake kula nyoka pamoja na nguo za
ndani kama sehemu ya huduma za Kanisa lake kwa Waumini… watu wa eneo
hilo waliwavamia na kumkamata Mchungaji huyo, Kanisa likaishia kuchomwa
moto, ambapo baada ya muda kidogo ilibidi Polisi waingilie kati
kumuokoa.
HUYU HAPA NDIYO WAZIRI MKUU WA TANZANIA KUTOKA BUNGENI..2015....
BREAKING
NEWS: Mh. Kassim Majaliwa Mbunge wa Ruangwa amependekezwa na Rais John
Magufuli kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Waziri Mkuu aliyependekezwa Mh. Kassim Majaliwa ni mbunge kupitia jimbo la Ruangwa na ana umri wa miaka 54.
Waziri Mkuu aliyependekezwa Mh. Kassim Majaliwa ni mbunge kupitia jimbo la Ruangwa na ana umri wa miaka 54.
TAIFA STARS..Kichapo cha Bao 7-0 kwa Taifa Stars dhidi ya Algeria kimemvunjia rekodi hii Mkwasa …
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars November 17 ilicheza mchezo wake wa pili wa marudiano ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2018 Urusi dhidi ya Algeria Blida katika uwanja wa Mustapha Tchaker na kukubali kipigo cha magoli 7-0, idadi ya magoli ambayo iliifanya Tanzania kuingia katika headlines ya ya kufungwa idadi kubwa ya magoli.
November 18 kocha wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa
ameongelea namna alivyokipokea kipigo hicho na kufanya kiweke historia
kwake kwani kwa miaka yake 25 katika soka hakuwahi kuweka rekodi ya
kupokea kipigo cha magoli mengi kiasi hicho kitu ambacho hakikuwaumiza
watanzania hata yeye.
“Kiukweli
hata mimi ilinishangaza kidogo na tulizidiwa umeona uwezo wa mchezaji
wao Yacine Brahimi uwezo wake ni mkubwa kikosi chao kilibadilika ila
uwanja pia ulikuwa tatizo ulikuwa unateleza hata goli la kwanza
tulilofungwa lilitokana na hivyo, kufungwa goli 7 sijawahi kiukweli
katika miaka 25 yangu katika soka” >>> Boniface Mkwasa
Wednesday, November 18
Rapa Mkali Toka Kitambo..Snoop Dogg aponda vikali orodha ya Billboard ya rappers wakali wa muda wote....
Rapa mkongwe duniani Snoop Dog ameponda vikali orodha
ya rapa wakali zaidi wa muda wote iliyotolewa na tovuti ya Billboard
wiki iliyopita.
Majina kwenye orodha hii yalikuwa pamoja na Biggie,
Jay Z, Eminem, Rakim, Nas, Andre 3000, Lauryn Hill, Ghostface Killah,
Kendrick Lamar na Lil Wayne.
Snoop Dogg amekasirishwa kuwa Tupac hakutajwa kwenye orodha hii. Haya ndio maneno yake kwenye instagram >>“This is so disrespectful. !!“Whoever did this list need a swift kick in the Ass. No. Tupac. Come on cuz ?. Jus my opinion.“
AGEUKA KIVUTIO ALGERIA...ANGALIA HUYU MWARABU ALIVYOKUWA AKIMUANGALIA SAMATTA....
HATIMAYE AIBUKIA KINONDONI....KMC FC YAANZA MAZUNGUMZO NA SELEMANI MATOLA....
Aliyekuwa Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola,
amethibitisha kuwa kwenye mazungumzo na Klabu ya Manispaa ya Kinondoni (KMC FC)
inayoshiriki Ligi Darala la Kwanza, lakini hofu imetanda klabuni hapo, kwani
imebainika haziivi na kocha wa timu hiyo, Amri Said ‘Jap Stam’ ambaye pia
aliwahi kuwa kwenye benchi la Simba msimu wa 2010.
Matola ambaye aliachana na Simba wiki iliyopita kwa
kile alichobainisha ni kutokuwa na maelewano mazuri na kocha mkuu, Dylan Kerr,
amesema amefanya mazungumzo na uongozi wa klabu ya KMC FC, lakini bado
hawajafikia muafaka.
“Wao walinifuata tukazungumza kiutendaji lakini
hakukuwa na muafaka katika mazungumzo yetu. Kama tutamalizana vizuri taarifa
zitatolewa tu na siyo jambo la kuficha,” alisema Matola.
Hata hivyo, kuonyesha kuwa uhusiano wake na Matola
siyo mzuri, Stam alipoulizwa kuhusu Matola kukaribia kujiunga na timu hiyo,
alisema:
“Sijaambiwa chochote kuhusu kumtaka Matola ingawa
taarifa hizo ninazo, kuwa wanataka tusaidiane kuhakikisha tunaipandisha timu
ligi kuu. Nafikiri hilo siyo jukumu lao ni jukumu la kocha mkuu, hivyo walikuwa
na kila sababu ya kunifuata kuniuliza kuhusu mtu sahihi katika kusaidiana
katika harakati hizi.
“Timu inafanya vema na dhamira yangu kuu ni kuipandisha
ligi kuu, hivyo kama ni masuala haya, wanataka kutibua hali ya mambo. Mimi
ndiye ninatakiwa kumtafuta msaidizi wangu na siyo mtu yeyote, maana mimi ndiye
kocha mkuu,” alifunguka kocha huyo aliyewahi pia kuzifundisha Mwadui na Ndanda.
SIKIA KAULI YA NAHODHA HUYU...ZLATAN KIBURI, JEURI! ATANGAZA KULISTAAFISHA SOKA TAIFA LOTE LA DENMARK......
Nahodha
wa Sweden, Zlatan Ibrahimovich amefunga moja kati ya mabao mawili
yaliyoiwezesha Sweden kusonga mbele katika kuwania kucheza Kombe la
Dunia baada ya kuing'oa Denmark.
Awali, Denmark walitamba kumstaafisha soka Zlatan, lakini baada ya sare ya 2-2, Sweden imesonga kwa jumla ya mabao 4-3 na Zlatan amesema: "Sasa taifa lao lote, nimelistaafisha soka."
Denmark na Sweden ni majirani ambao wana ushindani wa hali ya juu.
Denmark (4-2-3-1): Schmeichel 6.5; Jocobsen
6, Kjaer 5, Agger 6, Durmisi 5.5 (Vestergaard 83); Hojbjerg 6, Delaney 6.5
(Krohn-Dehli 45, 6); Poulsen 6.5, Eriksen 6, Jorgensen 6; Bendtner 5
Subs not used: Andersen, Wass, Kvist
Jorgensen, Braithwaite, Christensen, Falk Jensen, Simon Poulsen, Jakob Poulsen,
Rasmussen, Lossl.
Booked: Durmisi, Poulsen, Hojbjerg
Sweden (4-4-2): Isaksson 6.5; Lustig
6.5, Johansson 6, Granqvist 5.5, Bengtsson 5 (Olsson 86); Larsson 6.5
(Hiljemark 81), Lewicki 6.5, Kallstrom 6 (Svensson 69), Forsberg 6; Berg 6,
Ibrahimovic 8.5
Subs not used: Olsen, Helander,
Guidetti, Kujovic, Milosevic, Toivonen, Durmaz, Zengin, Carlgren.
Booked: Bengtsson, Larsson
Referee: Martin Atkinson (England) 6.5
KOCHA WA YANGA..PLUIJM ALIA CHALENJI KUHARIBU PROGRAMU NA KAMBI NZIMA.....
Yanga
imeshindwa kuingia kambini kujiandaa na Ligi Kuu Bara kutokana na
michuano ya Kombe la Chalenji iliyopangwa kuanza Novemba 20 jijini Addis
Ababa, Ethiopia.
Yanga hivi sasa inaendelea na maandalizi ya ligi kuu
chini ya Kocha Mkuu, Mholanzi, Hans van Der Pluijm na Juma Mwambusi wakati ligi
hiyo ikisimama.
Pluijm amesema ni
ngumu kuifuata programu aliyoipanga wakati ligi kuu ikisimama kutokana na nusu
ya wachezaji kuwepo vikosi vya timu zao za taifa.
Pluijm alisema, katika ripoti yake aliomba mechi tano
za kirafiki za kimataifa pamoja na kambi ya pamoja ya kujiandaa na ligi hiyo
katika kuhakikisha wanautetea ubingwa wao.
“Timu inaendelea na mazoezi yake ya pamoja ikiwa na
mchanganyiko wa wachezaji wa U20 baada ya nusu ya wachezaji wa timu kubwa
kuwepo kwenye timu zao za taifa.
“Hivyo hivi sasa siwezi nikafanya chochote ikiwemo kucheza mechi za kirafiki za kimataifa, pamoja na kambi ya kujiandaa na ligi kuu iliyosimama hadi pale wachezaji wote watakaporejea kujiunga na wenzao,” alisema Pluijm.
ETI LAZIMA WAONDOKE...BOMOA BOMOA MWENGE JIJINI DAR ES SALAAM LEO.......
Wananchi wakijaribu kuokoa mali zao baada ya maduka na nyumba kadhaa zilizojengwa isivyohalali kuvunjwa katika maeneo ya Mwenge jijini Dar es Salaam
Polisi Marekani yawatia nguvuni wanaharakati weusi...
Chini ya kaulimbiu “Black Lives Matter” waandamanaji hao walifunga barabara kuu ya Minnesota huku wakiwa wamebeba mabango na maberamu yaliyokuwa na jumbe za kulaani ubaguzi wa rangi.
Maandamano hayo yalinuia kuishinikiza polisi ya Minnesota kufafanua sababu za kuuawa kijana wa miaka 24 kwa jina Jamar Clack, mikononi mwa polisi katika jimbo hilo Jumapili iliyopita.
Subscribe to:
Posts (Atom)
















