Wednesday, November 18

Polisi Marekani yawatia nguvuni wanaharakati weusi...


Polisi Marekani yawatia nguvuni wanaharakati weusi
Maafisa wa polisi nchini Marekani wamewatia mbaroni zaidi ya wanaharakati 50 waliokuwa wakishiriki maadamano katika jimbo la Minnesota. Mamia ya wanaharakati hao wamefanya maandamano ya kukashifu dhulma wanazopitia watu weusi nchini humo.
Chini ya kaulimbiu “Black Lives Matter” waandamanaji hao walifunga barabara kuu ya Minnesota huku wakiwa wamebeba mabango na maberamu yaliyokuwa na jumbe za kulaani ubaguzi wa rangi. 
Maandamano hayo yalinuia kuishinikiza polisi ya Minnesota kufafanua sababu za kuuawa kijana wa miaka 24 kwa jina Jamar Clack, mikononi mwa polisi katika jimbo hilo Jumapili iliyopita.

No comments: