Wednesday, November 18

Je Ni Sawa kusikiliza muziki wa R Kelly baada ya kujua alikuwa na mahusiano na binti mwenye miaka chini ya 18 ?.....



r kelly
Kuelekea kutoka kwa album yake ya 13 ‘The Buffet’ rnb staa R Kelly amefanyiwa mahojiano hivi karibuni na jarida la New York  kuhusu tabia na skendo yake ya zamani ya kuwa na mahusiano na mabinti wenye umri chini ya miaka 18.
Swali kubwa lilikuwa Je Ni Sawa kusikiliza muziki wa R Kelly baada ya kujua au kudhani anatabia hii ?
Kila siku ni takuwa ni zawadi kwa watu ila hilo litabaki kuwa laana kwangu, watu milioni moja wananiongelea vibaya ila milioni nane wananipenda,so nina watu milioni tisa wanaoniongelea,hio inanifanya nizidi kubaki kwenye muziki “.
Mwandishi wa habari za burudani mjini Chicago alifanyiwa mahojiano na jarida hili pia na kusema ” Sio sahihi kuhusisha maisha binafsi ya msanii na Muziki au sanaa yake, kama unapenda sanaa yake baki kuwa shabiki “.
R Kelly pia ameulizwa kama bado anatamani kuwa na mabinti wenye umri chini ya miaka 18 ?
Kelly alijibu kwa kusema ” huo ni uzushi kama uvumi mwingine tu duniani, ndio maana siongelea mambo hayo, ningekuwa mtu wa kawaida haya mambo yasingeongelewa kuhusu mimi  “.

No comments: