Wednesday, November 18

JESHI IMARA...CAR yataka isaidiwe kuimarisha jeshi lake....


CAR yataka isaidiwe kuimarisha jeshi lake
Mkuu wa Baraza la Mpito la Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ferdinand Alexandre Nguendet ameitaka jamii ya kimataifa kuisaidia nchi yake kuimarisha uwezo wa jeshi ili kukabiliana na hali mbaya ya kiusalama katika nchi hiyo. 
Nguendet amefafanua kuwa, serikali ina mpango wa kuwachukua vijana 1000 kutoka kila jimbo na kuwapa mafunzo ya kijeshi na kwa njia hiyo taifa litaweza kupata jeshi jipya na imara. 
 Jamhuri ya Afrika ya Kati ina majimbo 77 na endapo mpango huo wa serikali utatekelezwa, jeshi jipya la nchi hiyo litakuwa na wanajeshi elfu 77. 
 Ferdinand Alexandre Nguendet amesema njia pekee ya kurejesha amani na utulivu Jamhuri ya Afrika ya Kati ni kuwa na jeshi imara na lenye uwezo wa kulinda mipaka ya nchi lakini pia kudhibiti hali ya mambo ndani ya nchi.

No comments: