Wednesday, November 18

Wanachama wa Boko Haram mikononi mwa Cameroon..... Cameroon yawakamata wanachama wa Boko Haram

Jeshi la Cameroon limetangaza kuwa limewatia nguvuni wanachama kadhaa wa kundi la kigaidi la Boko Haram.
Cameroon yawakamata wanachama wa Boko HaramJeshi hilo limesema wanachama hao 19 wa kundi la Boko Haram wametiwa nguvuni katika kitongoji cha Ketta karibu na mpaka wa nchi hiyo na Nigeria katika operesheni iliyofanywa na jeshi la anga na la nchi kavu la nchi hiyo.
Vyombo vya jeshi la Cameroon vimesema kuwa idadi nyingine ya wapiganaji wa kundi la kigaidi la Boko Haram imeangamizwa katika mashambulizi yaliyoendelea kwa kipindi cha masaa mawili.
Jeshi la Cameroon lilianzisha operesheni kali ya kuwasaka na kuwaangamiza wanachama wa kundi la kiwahabi na kigaidi la Boko Haram baada ya wanachama wake kuvamia eneo la kaskazini mwa nchi hiyo na kuua idadi kubwa ya raia wa eneo hilo.  

No comments: