Washukiwa wawili
wamefariki baada ya maafisa wa usalama kushambulia Saint Denis kaskazini
mwa Paris, wakisaka waliohusika mashambulio ya Ijumaa.
Ufyatulianaji
mkali wa risasi umetokea mapema asubuhi kwenye mtaa huo. Operesheni
hiyo inadaiwa kumlenga mwanamgambo wa Islamic State Abdelhamid Abaaoud
ambaye amedaiwa kupanga mashambulio hayo yaliyoua watu 129.Maafisa kadha wa polisi wamejeruhiwa kwenye operesheni hiyo, kituo cha runinga cha BFMTV cha Ufaransa kimeripoti.
Naibu meya Stephane Peu amewahimiza raia wasalie manyumbani, akisema "hili si shambulio jipya bali ni operesheni ya polisi".
Awali, duru za kiusalama zilisema video ya kiusalama ilikuwa imeonyesha huenda kulikuwa na mshambuliaji wa tisa mashambulio hayo ya Ijumaa.
Watu 129 walifariki kwenye mashambulio yaliyotokea maeneo sita mjini Paris.
Kundi la Islamic State (IS) limesema ndilo lililotekeleza mashambulio hayo.
Ripoti moja inasema barabara zimefungwa eneo la Place Jean Jaures mtaa wa Saint Denis.
No comments:
Post a Comment