Gazeti la L’Observanteur la nchi hiyo limesema kuwa Rais Macky Sall ametia saini sheria hiyo, kufuatia mashinikizo kutoka kwa taasisi za kiusalama na kiulinzi za nchi hiyo.
Hii ni katika hali ambayo, katika mkutano wa usalama na amani wa bara Afrika uliofanyika Jumatatu iliyopita mjini Dakar, Rais Sall alidokeza kuwa vazi hilo linafanya vita dhidi ya ugaidi kuwa vigumu.
Miezi michache iliyopita, Cameroon nayo ilipiga marufuku vazi hilo la heshima la Kiislamu.
Viongozi wa Cameroon walichukua uamuzi huo baada ya kujiri mlipuko uliouwa watu 13 na kujeruhi wengine 31 mwezi Julai mwaka huu.
No comments:
Post a Comment