Thursday, April 14

BARCELONA NI KAMA SIMBA YA BONGO, YATUPWA NJE UEFA NA MAJIRANI WA MAHASIMU WAO JIJINI MADRID


Hivi majuzi timu y asoka y aSimba SC ya hapa nyumbani iling'olewa katika hatua y arobo fainali katika kombe la FA licha ya mashabiki wengi kuipa nafasi y akushinda kutokana na mwenendo mzuri iliyonayo katika ligi, lakini mbele ya Vijana wa Tanga, {Coastal Union} wakalala mbili moja mwele ya mashaiki wao jijini Dar es salaam.

vivyo hivyo hapo jana usiku Klabu ya soka ya Barcelona Jumatano ilivuliwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Atletico Madrid huku Mabao yote ya Altletico Madrid yakifungwa na Antoine Griez-mann na bao la pili likifungwa kwa mara nyingine na Antoine kwa njia ya penalti .

Kwa matokeo hayo Atletico Madrid wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 3 -2 baada ya awali kufungwa 2-1 na Barcelona katika Uwanja wa Camp Nou.

Katika mchezo mwingine Bayern Munich imefakiwa kutinga nusu fainali baada ya kuitoa Benfica kwa ushindi wa jumla wa 3-2 baada ya sare ya 2-2 katika mchezo wa jana .

Mabao ya Benfica yamefungwa na Raul Alonso Rodriguez na Anderson Souza Conceicao , na magoli ya Bayern Munich yakifungwa na Arturo Vidal na Thomas Muller .

Hivyo Atletico Madrid na Bayern Munich zinaungana na Real Madrid ya Hispania pamoja na Manchester City katika nusu fainali ambayo droo yake itapangwa siku ya Ijumaa.

Wednesday, April 13

KAMANDA WA POLIS MWANZA AWATAKA POLIS KUWAKABILI MAJAMBAZI KWA NGUVU ZOTE....


Kamanda mpya wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Ahmed Msangi amewataka polisi kukabiliana na majambazi kwa nguvu zote na ikibidi kuwaua kabla hawajasababisha madhara makubwa kwa raia.

NEC YAPONGEZWA KWA UCHAGUZI WA 2015 KUMALIZIKA KWA AMANI


Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala imeipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kufanikisha kuendesha Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani wa mwaka 2015 vizuri na kuiacha nchi ikiwa na Amani, utulivu na Usalama.

WANANCHI WATAKIWA KUWAOMBEA VIONGOZI

 

MKE wa Waziri Mkuu, Mary Majaliwa amewaomba wananchi wa wilaya ya Ruangwa kuwaombea dua viongozi wa taifa, Rais Dk. John Magufuli, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ili waweze kufanya kazi zao kikamilifu. 

PICHA !! RAIS MAGUFULI AKIPOKEA HATI ZA UTAMBULISHO WA MABALOZI KUTOKA NCHI MBALIMBALI IKULU

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati ya Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa nchi ya Jamhuri ya Czech hapa nchini Pavel Rezac, tukio hilo lilifanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Monday, April 4

SHINIKIZO LA KIMATAIFA KUHUSU ZANZIBAR BADO LINAINYEMELEA TANZANIA


Siku chache baada ya Shirika la Changamoto za Milenia (MCC), kufuta Tanzania kwenye nchi wanachama wake na hivyo kuikosesha serikali msaada wa zaidi ya Sh. trilioni moja kutokana na uchaguzi wa Zanzibar, Umoja wa Ulaya (EU), upo hatarini kutotoa Sh. trilioni 1.56 kwa sababu ya suala hilo huku mmoja wa Waziri wa Uingereza, akiitaka serikali yake isitoe Sh. bilioni 622 za msaada kwa Tanzania.

KAMATI YA MISS TANZANIA YAZINDUA MSIMU MPYA WA MASHINDANO YA MISS TANZANIA 2016 JIJINI ARUSHA

Hashim Lundenga
Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa shindano la Miss Tanzania, Hashim Lundenga (kulia) akimiminiwa kinywaji cha K-Vant wakati wakiingia na wadau wa tasnia ya urembo kwenye ukumbi wa Triple A jijini Arusha wakati wa uzinduzi wa msimu mpya wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania 2016 uliofanyika mwishoni mwa juma.

ANASWA AKISAFIRISHA SMG NDANI YA BASI LA ABIRIA MOROGORO


Polisi  mkoani Morogoro inamshikilia Juma George (29) mkazi wa Shinyanga, kwa kukutwa na silaha ya kivita aina ya SMG iliyofutwa namba zake za usajili, magazini mbili, risasi 21 pamoja na panga vikiwa vimehifadhiwa ndani ya begi lake la nguo.

CUF KUTOA MSIMAMO WAO LEO KUHUSU HALI YA ZANZIBAR

Chama kikuu cha upinzani visiwani Zanzibar leo kinatarajiwa kutangaza mikakati yake na msimamo kuhusiana na mzozo wa kisiasa wa Zanzibar.
Hata hivyo msimamo huo unatarajiwa kuzungumzia mufaka katika ya chama cha CUF na CCM ambao ulileta uundwaji wa serikali kati ya vyama hivyo viwili.
Chama cha CUF visiwani Zanzibar bado kinaendeleza msimamo wake kususia kutambua matokeo na serikali iliyoundwa kufuatia uchaguzi wa marudio.
Hivi karibuni shirika la misaada la Marekani MCC lilisitisha msaada wa dola 487 kwa madai ya kutoridhishwa na hali ya kisiasa visiwani Zanzibar.

DKT. KIGWANGALLA AFUNGUA OFISI MPYA ZA SHIRIKA LA T-MARC TANZANIA.

1T
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla Charles Singili Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la T. Marc Tanzania pamoja na Diana Kisaka Mkurugenzi wa Shirika la T.Marc Tanzania wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa ofisi za shirika hilo zilizoko Kunduchi jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki , Shirika hilo linajihusisha na shughuli mbalimbali ikiwemo utoaji wa elimu katika masuala ya ukimwi, Malaria na Elimu ya Uzazi.

WAJASIRIAMALI DAR WAJAZWA MADINI KUHUSU FURSA MPYA KATIKA KILIMO BIASHARA

Margareth Nzuki - ESRF
Mkuu wa Idara ya Maarifa na Ubunifu wa ESRF, Bi. Margareth Nzuki akiwasilisha malengo ya warsha kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dk. Tausi Kida kufungua warsha hiyo.

Saturday, April 2

WAZIRI NAPE AFANYA MKUTANO NA WASAMBAZAJI WA FILAMU NA MUZIKI NCHINI LEO

ep1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye akiongea na wasambazaji wa filamu na muziki nchini wakati wa mkutano kati yake na wasambazaji hao uliojadili namna gani ya kuboresha tasnia hiyo kwa manufaa ya wasanii, wasambazaji na uchumi wa Taifa.(Picha Na Benjamin Sawe- WHUSM)

WAFANYAKAZI WA DAWASCO WAFANYA USAFI HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Majisafi na Maji taka Dar es Salaam (Dawasco ) Mhandisi Cyprian Luhemeja akishiriki zoezi la usafi katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili na watumishi wa Dawasco.

KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE YAKUTANA KUTATHIMINI KAZI ZA KAMATI ZA BUNGE

KM1
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akiteta jambo na Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati cha Kamati ya Uongozi ya Bunge leo tarehe 2/42016 Ofisi ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.Kamati hiyo inayojumuisha Wenyeviti wote wa Kamati za Kudumu za Bunge ilikutana ili kufanya thathmini ya shughuli za kamati za Kudumu za Bunge kabla ya Serikali kuwasilisha Mapendekezo ya Mpango na ukomo wa Bajeti ya mwaka 2016/17 wiki ijayo.

WABUNGE BARANI AFRIKA WAKUTANA NA KUJADILI JINSI YA KUPINGA BIASHARA HARAMU YA SILAHA AFRIKA

LIA1
Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiwahutubia baadhi ya Wabunge kutoka nchi mbalimbali za Afrika wakati wa Mkutano wa kujadili namna gani nchi za Afrika zinavyoweza kupinga biashara haramu ya silaha, leo Jijini Dar es Salaam

MKUU WA WILAYA YA SIHA AONGOZA WANANCHI KUPANDA MITI SIKU YA MAZINGIRA

Mkuu wa wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro ambaye pia anakaimu wilaya ya Hai,Dk Charles Mlingwa akizungumza na wananchi wakati wa maadhimisho ya mazingira kwenye chanzo cha uzalishaji umeme cha Kikuletwa kinachosimamiwa na Chuo cha Ufundi Arusha(ATC),kushoto ni Makamu wa Chuo hicho(Utawala na Fedha)Mhandisi Dk Erick Mgaya.

NAIBU KATIBU MKUU CCM AENDELEA NA ZIARA MAFINGA MKOANI IRINGA LEO

IR1
Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara), Rajab Luhwavi akilakaiwa na Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Iringa, Elisha Mwampashi ambaye ni Katibu wa CCM wilaya ya Iringa Mjini, alipowasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Mufindi katika mji mdogo wa Mafinga leo April 2, 2016, akiwa katika ziara ya kikazi, kuzungumza na watumishi wa Chama ili kusikiliza changamoto na kero zinazowakabili. Kulia ni Katibu wa CCM Wilaya ya Mufindi Jimson Mhagama. (Picha na Bashir Nkoromo).

Saturday, March 12

MRADI WA PARTOMA WATOA MATOKEO YA UTAFITI WA WODI ZA WAZAZI

pat1

Mwenyekiti wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Kanga Meternity Trust (KMT) Dkt. Mohd Hafidh akitoa maelezo ya taasisi hiyo inavyofanya kazi zake kuhakikisha Mama wajawazito wanapata huduma bora wanapokwenda kujifungua hospitali Kuu ya Mnazimmoja katika hafla ya  kuwasilishwa  Utafiti wa Mradi wa PartoMa iliyofanyika Hoteli ya Tembo, Forodhani Mjini Zanzibar.
pat2
Madaktari bingwa wa Hospitali ya Mnazimmoja Dkt. Naufal Kassim (kushoto), Dkt. Zaki (kati) na Mwenyekiti wa KMT Dkt. Mohd Hafidh wakijadiliana jambo wakati wa hafla ya kuwasilishwa utafiti uliofanywa na Dkt. Anna Maaloe (hayupo pichani) kuhusu wadi za wazazi za Hospitali ya Mnazimmoja.
pat3
Mtafiti kutoka Mradi wa PartoMa Dkt. Anna Maaloe akiwasilisha utafiti wake juu ya huduma za wodi za wazazi za Hospitali kuu ya Mnazimmoja katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Tembo Forodhani Mjini Zanzibar.
pat4
Mwenyekiti wa Baraza la wauguzi na wakunga Dkt. Amina Abdulkadir akitoa mchango wake wakati wa kuwasilishwa utafiti wa huduma za wodi za wazazi za Hospitali kuu ya Mnazimmoja. Picha na Makam Mshenga-Maelezo Zanzibar.
pat5
Dkt. Ali Salum kwa niaba ya  Mkurugenzi wa Hospitali kuu ya Mnazimmoja akimkabidhi cheti na zawadi Metroni Mkuu  wa Hospitali hiyo kwa kushiriki mafunzo ya kuwajengea uwezo yaliyoandaliwa na Mradi wa PartoMa katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Tembo.
pat6
Wauguzi wa wodi ya wazazi katika Hospitali Kuu ya Mnazimmoja wakimpa zawadi ya mlango na kasha Dkt. Anna  Maaloe kwa kazi nzuri aliyosimamia ya utafiti wa wodi za wazazi katika Hospitali ya Mnazimmoja. Picha na Makam Mshenga-Maelezo Zanzibar.
………………………………………………………………………………………………………………………
Na Ramadhani Ali/Maelezo Zanzibar   
Mradi wa PartoMa unaoshirikisha  Chuo Kikuu cha Copenhagen nchini  Denmark na Hospitali Kuu ya Mnazimmoja   wenye lengo la kuongeza ufanisi na kuwajengea uwezo   wafanyakazi  wa  wodi  za wazazi katika hospitali ya Mnazimmoja umeanza kuleta  mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na mradi wa PartoMa kwa kushirikiana na Taasisi isiyo ya kiserikali Kanga Martenity Trust (KMT) iliyopo Hospitali ya  Mnazimmoja umeonyesha vifo vinavyotokana na  uzazi  na vifo vya watoto wanaozaliwa vimepungua tokea kuanza kwa mradi huo mwaka mmoja uliopita.

Akiwasilisha utafiti uliofanywa  na mradi wa PartoMa ambao uliwashirikisha madaktari, wakunga na wasaidizi wakunga katika wodi za wazazi, Dkt. Anna Maaloe amesema bado ni mapema kuthibitisha kuwa mafanikio hayo yanatokana moja kwa moja na kuwepo  mradi huo lakini ufanisi na utaalamu wa wafanyakazi  kwenye wodi za wazazi  Hospitali ya Mnazimmoja umeongezeka.

Amesema Hospitali za rufaa, kama ya Mnazimmoja zinawajibu mkubwa wa kuwa na mafunzo ya mara kwa mara kwa wafanyakazi waliopo na wanaotegemewa siku za mbele na kuweka miongozo bora ili kuokoa maisha ya mzazi na mtoto pamoja na wagonjwa wa kawaida.

“Kwa kuliona hilo mradi wa PartoMa umekuwa ukiandaa mafunzo  ya kuwajengea uwezo   madaktari na watendaji wa wodi za wazazi   Hospitali  Mnazimmoja siku moja kwa  miezi mitatu baada ya saa za kazi  na kuweka miongozo  ambapo  wafanyakazi wengi wamekuwa wakishiriki,” aliongeza Dkt. Anna.

Katika utafiti huo  Dkt.  Anna amesema imebainika kuwa wafanyakazi wengi wa Hospitali  ya Mnazimmoja wamehamasika kuongeza elimu na ufanisi na hiyo inasaidia katika kuokoa maisha ya  wananchi.

Hata hivyo amesema bado kunachangamoto katika kutoa huduma bora zaidi katika Hospitali ya Mnazimmoja ikiwemo  uhaba wa wafanyakazi katika wodi za wazazi ukilinganisha  na ongezeko kubwa la wazazi wanaotumia Hospitali hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Hoteli ya Tembo Forodhani, Mwenyekiti wa KMT Dkt. Mohammed Hafidh amesema utafiti huo ambao ni wa kwanza kufanywa na kuwashirikisha watafiti wa wazalendo  Hospitali ya Mnazimmoja utasaidia kuwa na taarifa sahihi na za uhakika kwa maendeleo ya Hospitali hiyo.

Amesema lengo la utafiti huo ni kuwasaidia mama wajawazito  kujifungua salama na kwa heshma na kuzuia vifo vya mama na mtoto ambavyo vinaweza kuzuilika.

Nae Dkt. Naufal Kassim amekiri kuwepo mtafartoMa  na ameshauri madaktari kujipanga kufanya tafiti zaidi za afya na kuyatumia  matokeo ya tafiti zilizopo kwa ukamilifu.

Katika hafla hiyo  Dkt. Ali Salum kwa niaba ya Mkurugenzi wa Hospitali Kuu ya Mnazimmoja aliwakabidhi  vyeti madaktari, wakunga na wasaidizi wakunga walioshiriki    mafunzo ya kuwajngea uwezo   baada ya saa za kazi  bila malipo katika hospitali hiyo.

WAKANDARASI WA MRADI WA MAJI MKOANI KIGOMA WABANWA .

 

 Naibu waziri wa maji na umwagiliaji mhandisi Izack Kamwele akikagua chanzo kikuu cha maji safi na salama cha mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji katika mji wa kigoma kilichopo eneo la katonga.

Friday, March 11

MARCO ROBIO AMSHAMBULIA TRUMP

Muwania urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Marco Rubio amemshambulia mwenzake Donald Trump kwa kusema kuwa Uislam unaichukia Marekani, katika mdahalo uliorushwa kwenye televisheni huko Miami.