Monday, July 13

Afisa usafirishaji ajitosa kuwani Udiwani kata ya Luhota jimbo la Kalenga

KATIBU wa uchumi na fedha wa chama cha usafirishaji Mkoani Iringa, Obedi Luhwago ameamua kujitisa kuwania udiwani katika kata ya Luhota, jimbo la Kalenga wilayani Iringa kwa tiketi ya Chama Cha Mapnduzi (CCM).
 
Akizungumza na Uhuru, Mtove alisema kuwa ameamua kuwani nafasi hiyo ili aweze kushirikiana na wananchi wa kata hiyo katika kuleta maendeleo.

Alisema lengo lake ni kuhakikisha anasimamia kwa ufasaha utekelezaji wailani ya CCM kwenye kata hiyo endapo, chama chake kitampa ridhaa ya kukimbiza bendera kwenye kata hiyo.

“Nimeamua kutangaza nia baada ya baraza la madiwani kuvunjwa kwa sababu tayari filimbi imepiga kelele, ninayo nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa kata ya Luhota,”alisema.

Luhwago alisema angeweza kuwania kata ya mjini ambako hivi sasa anaishi, lakini kutokana na mahitaji ya nyumbani kwao, ameamua kurejea kijijini, ili aweze kuwania kata yao.

Aliwaomba wananchi wa kata hiyo kumuunga mkono wakati utakapofika, kwa madai kuwa kwa ushirikiano wao wanaweza kusogeza gurudumu la maendeleo.

Akizungumzia upinzani, Luhwago alisema kuwa wananchi wanaimani kubwa na CCM kutokana na utekelezaji wake wa ilani, katika kipindi kinachoisha.

“Viongozi wanaomaliza muda wao wamefanya kazi na kuleta imani ya chama kwa wananchi, kwa sababu hiyo CCM itaendelea kushika hatamu katika uchaguzi ujao, na wapinzani hawataambulia chochote,” alisema.

Kumekuwa na wimbi kubwa na wana CCM kujitisa kwenye chaguzi mbalimbali jambo ambalo linaonyesha kukuwa kwa demokrasia.

No comments: