Friday, July 17

HIZI HAPA TWEETS ZA MASHABIKI WA ARSENAL WAKI-REACT STORI YA GUNNERS KUMSAJILI STRAIKA HUYU....

Mashabiki wa Arsenal wameamka asubuhi ya leo na kukutana na stori ambayo inaihusisha klabu yao kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Karimu Benzema.

Habari hiyo imeandikwa ukurasa wa nyuma wa gazeti la The Sun akisema kwamba Arsenal wapo tayari kulipa dau la paundi milioni 40.

The Sun wameongeza kwamba Arsene Wenger yuko tayari kulipa dau hilo mapema Jumatatu ijayo.

Je, Safari hii stori ni nini? kwanini tuamini kwamba Arsenal wanaweza kumsajili Benzema majira haya ya kiangazi?

Wiki kadhaa zilizopita, Gazeti la AS la Hispania liliripoti kwamba kocha wa Real Madrid, Rafa Benitez anataka kubadili mfumo wa uchezaji wa klabu hiyo kuanzia msimu ujao.
Katika ripoti hiyo ilielezwa kwamba msimu ujao Cristiano Ronaldo atacheza kama mshambuliaji wa kati kwasababu Benitez anapendelea mfumo wa 4-2-3-1.
Zaidi, gazeti hilo lilisema kwamba Benzema mwenye umri wa miaka 27 hatapenda kucheza msimu ujao akianzia benchi.
Sasa tetesi zimeenea kwamba Arsenal wameanza kuongea na viongozi wa Benzema kuona uwezekano wa kumsajili na ndio maana gazeti la The Sun limekuja na stori hiyo leo.

Hapa chini ni baadhi ya Tweets baada ya Arsenal kuhusishwa kumsajili Benzema;



No comments: