Friday, July 17

VAN GAAL ASEMA HAYA KUHUSU USAJILI.

Meneja wa Manchester United,  Louis van Gaal amethibitisha kwamba bado anahitaji kusajili wachezaji wawili majira haya ya kiangazi licha ya ukweli kuwa ameshanasa saini ya wachezaji wanne mpaka sasa.
Van Gaal ametumia paundi milioni 80 kumsajili winga wa  PSV Eindhoven, Memphis Depay, beki wa kulia wa Torino, Matteo Darmian na viungo Bastian Schweinsteiger kutoka Bayern  na Morgan Schneiderlin Southampton.
Mholanzi huyo ameiambia MUTV kuwa bado ana mapengo mawili katika kikosi chake.
"Hapana, hatujamaliza usajili". Amesema Van Gaal na kuongeza: " Tutanunua mchezaji ambaye anaweza kuleta mchango, nadhani bado tunahitaji kuongeza wachezaji wawili katika sehemu mbili na tutafanya hivyo pale inapowezekana".
Van Gaal  pia anamuwinda mlinzi wa kati Sergio Ramos, lakini dau la paundi milioni 40 alilotuma Real Madrid limekataliwa mara kadhaa, wakati huo inaelezwa kwamba Man United wanataka kumuuza Jonny Evans.
Van Gaal amesema kwamba Javier Hernandez "Chicharito" atakuwa sehemu ya kikosi chake.

No comments: