Monday, July 13

ROONEY, BALE?,ANGALIA ORODHA YA WACHEZAJI WA KIINGEREZA WALIOWAHI KUSAJILIWA KWA GHARAMA KUBWA ZAIDI

Ofa iliyokubaliwa ya Manchester City kumsajili kiungo Raheem Sterling kutoka klabu ya Liverpool imeweka rekodi mpya katika orodha ya wachezaji ghali zaidi wenye asili ya taifa la Uingereza.


Man City wamekubali kuilipa Liverpool ada ya kiasi cha paundi milioni 49 kwa ajili ya kumnasa Sterling na kumfanya kuwa mchezaji ghali zaidi ambaye bado yupo chini ya umri wa miaka 21.
Raheem Sterling sasa anashika nafasi ya pili nyuma ya Gareth Bale aliyeuzwa miaka miwili iliyopita kwa ada iliyovunja rekodi ya Dunia ya paundi millioni 85.3 – akitokea Tottenham kwenda Madrid.
Andy Carrol anashika nafasi ya 3 kwa kuuzwa kiasi cha paundi millioni 35 akitokea Newcastle kwenda Liverpool.

Rio Ferdinand alinunuliwa na Manchester United akitokea Leeds United kwa Paundi milioni 30 na kuweka rekodi ya kuwa beki ghali zaidi kuwahi kutokea kwa kipindi hicho.
Orodha kamili ya Wachezaji ghali zaidi wa Kiingereza
Paundi milioni 85.3 – Gareth Bale (Tottenham kwenda Real Madrid, 2013)

Paundi milioni 49* – Raheem Sterling (Liverpool kwenda Manchester City, 2015) * nuhamisho bado haujakamilika lakini.
Paundi Milioni 35 – Andy Carroll (Newcastle kwenda Liverpool, 2011)
Paundi milioni 30 – Rio Ferdinand (Leeds kwenda Manchester United, 2002)
Paundi milioni 27 – Luke Shaw (Southampton kwenda Manchester United, 2015)

Paundi milioni 27 – Wayne Rooney (Everton kwenda Manchester United, 2004)

Paundi milioni 26 – James Milner (Aston Villa kwenda Manchester City, 2010)

No comments: