Friday, September 18

MWAMERIKA ALIYEENDA KUTOA MSAADA KWA WAHANGA WA TETEMEKO ASIKITISHA WATU KWA KILICHOMKUTA!! FUATILIA KISA KIZIMA HAPA {VIDEO}

Dahlia Yehia alikuwa ni msichana mwenye furaha, amani na moyo wa kuwasaidia watu wenye shida lakini ndoto zake zilifupishwa baada ya safari yake ya kwenda Nepal kwenda vibaya!

NIMEONA NIKULETEE MIJENGO YA HOTEL ZA AJABU ZINAZOPATIKANA HUMU DUNIANI........


Teknolojia ya sasa inazidi kukua siku hadi siku, wataalamu wamekuwa wakibuni vitu mbalimbali duniani kwa lengo la kuleta ushindani.

WIZARA YA AFYA YAMTAKA MKEMIA MKUU ATAFUATILIA MATUMIZI YA SIGARA YA KIKO YA MAJI (SHISHA)

index 
 
………………………………….
WIZARA ya Afya na Ustawi wa Jamii imeiagiza Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kufuatilia matumizi ya sigara ya kiko ya maji (Shisha) katika kumbi za starehe  za hapa nchini kwa kuwa sigara hizo zinahusishwa na  matumizi ya madawa ya kulevya.

USHAWAHI KUSIKIA NDOA YA FASTA FASTA? SASA HII IMEFUNGIWA BEACH MBELE YA WATU NANE......SOMA NA TAZAMA PICHA HAPA


Ronke na Lawson wamependana? Love yao hawakutaka masuala ya kusumbuana na ndugu masuala ya michango, vikao vya Harusi, kujaza watu Ukumbini.. wao kila kitu kimefanywa simple tu yani.

SERIKALI YAUJIBU UKAWA KUHUSU SAFARI YA RAIS NA GHARAMA,YADAI KUTOTUMIA HATA NUSU YA KIWANGO WALICHOKITAJA WAPINZANI

TAARIFA KWA UMMA - ZIARA ZA RAIS NJE

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 

Safari za Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete Nje ya Nchi.
 

Wizara imesikitishwa na taarifa za uongo zilitolewa katika vyombo vya habari kuwa Mhe. Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uongozi wake wa miaka 10 ametumia Shilingi trilioni 4 kwa ajili ya safari za kikazi nje ya nchi, ambazo ni wastani wa bajeti nzima ya wizara kwa miaka mitano (5).

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa inapenda kutoa ufafanuzi kuwa tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete aingie madarakani mwaka 2005, kiasi kikubwa kabisa cha bajeti kuwahi kutengwa kwa ajili ya safari za Viongozi Wakuu yaani Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu ni shilingi bilioni 50 ambazo zilitengwa kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015 kwa ajili ya Idara ya Itifaki. 


Kwa miaka mingine yote wastani umekuwa ni kati ya shilingi bilioni tano hadi 25 kulingana na mahitaji ya idara hiyo.
 

Ifahamike kuwa kiasi hicho cha shilingi bilioni 50 ni bajeti nzima ya Idara ya Itifaki, ambapo kuna fungu maalum kwa ajili ya ziara za viongozi. Fungu hilo linagharamia makundi makuu matano kama ifuatavyo:
 

1. Kundi la Rais wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au Wakuu wa Taasisi na Walinzi;
 

2. Kundi la Makamu wa Rais wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au Wakuu wa Taasisi na Walinzi;
 

3. Kundi la Waziri Mkuu wakiwemo Wasaidizi, Mawaziri au Wakuu wa Taasisi na Walinzi;
 

4. Kundi la Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka nje ya nchi wanapotembelea Tanzania; na
 

5. Kundi la Wajumbe Maalum wanaokuja nchini kuleta taarifa muhimu kwa Rais.
 

Makundi yote haya hugaramiwa na Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ndani ya bajeti ya Idara ya Itifaki kifungu cha Ziara za Viongozi.

Aidha uandaaji wa bajeti ya Wizara chini ya Idara ya Sera na Mipango unahusisha wadau wengine nje ya Wizara kama vile Kamati ya Bunge ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na hupitishwa kila mwaka na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Tunapenda kuwaatahadharisha wananchi juu ya watu wanaotoa taarifa za uongo kwa madhumuni ya kujenga chuki dhidi ya Serikali. Ikumbukwe kuwa ziara za viongozi zinazoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje zina mafanikio makubwa kwa nchi na Watanzania kwa ujumla.

Wizara inaandaa taarifa ya ndefu ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara, changamoto na mafanikio yaliyopatikana ndani ya kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambayo itatolewa kwa umma kwa lengo la kutoa elimu zaidi.
 

                                                                                        Imetolewa na:
                                                    Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
                                             Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
                                                                                  17 Septemba 2015

Queen Darleen: Muziki Umenikosanisha Na Boyfriends Zangu

Queen Darleen ambaye pia ni dada yake na Diamond amesema ameachana na wanaume wengi kutokana familia za wanaume kutomkubali kwa kudai ni mhuni.
11264967_899675290067888_1156573801_n 
Darleen alisema ndugu wa upande wa wanaume wamekuwa wakichochotea maneno kwa watoto wao hali iliyosabisha kuachana.

Saturday, August 8

Friday, July 17

Chuck Norris huyu hapa full movie kazi kwako

UNAIKUMBUKA HII A WORRIORS JOURNEY YA BRUCE LEE? ITAZAME HAPA

HIZI HAPA TWEETS ZA MASHABIKI WA ARSENAL WAKI-REACT STORI YA GUNNERS KUMSAJILI STRAIKA HUYU....

Mashabiki wa Arsenal wameamka asubuhi ya leo na kukutana na stori ambayo inaihusisha klabu yao kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Karimu Benzema.

MSIKIE PLUIJM WA YANGA ANAVYOINGIA KESHO UWANJANI DHIDI YA GOR MAHIA KOMBE LA KAGAME

Kocha wa Yanga SC Hans van der Pluijm (kulia) akiwa na kocha wa Gor Mahia Frank Nuttal (kulia) walipozungumza na Waandishi wa Habari mchana huu

TAZAMA VIDEO YA JAMES MILNER AKIFUNGA GOLI LA KWANZA LIVERPOOL IKIFANYA MAANGAMIZI LEO....

TANZIA: MSANII MKUBWA WA MUZIKI WA BENDI AFARIKI DUNIA...


Mwanamuziki wa muziki wa bendi Ramadhan Masanja maarufu kama 'Banza stone' amefariki dunia nyumbani kwao hivi punde baada ya kuugua kwa muda mrefu.
R.I.P Banza Stone

VIDEO::HIVI NDIVYO BAYERN WALIVYOPOKELEWA BEIJING LEO

UNADHANI BONGO KUNA PRO ANAWEZA KUPOKELEWA NAMNA HII KAMA MAPOKEZI YA DEPAY

Nyota wa Manchester United Memphis Depay akiwasainia mashabiki wa timu hiyo vitu mbalimbali  ikiwemo mipira na jezi wakati wa ziara yao nchini Canada katika maandalizi ya msimu mpya wa ligi.

VAN GAAL ASEMA HAYA KUHUSU USAJILI.

Meneja wa Manchester United,  Louis van Gaal amethibitisha kwamba bado anahitaji kusajili wachezaji wawili majira haya ya kiangazi licha ya ukweli kuwa ameshanasa saini ya wachezaji wanne mpaka sasa.

SINA UHAKIKA KAMA HUYU ANAWEZA KURITHI VIATU VYA IKER CASILLAS

Real Madrid wamethibitisha kumsajili Golikipa wa Espanyol,  Kiko Casilla.

MRUNDI HUYU AME-COMMENT HIVI KUHUSU KOCHA WA AZAM

Stewart Hall (kulia) 

MESSI AMECHORA TATOO ZA AINA MBALIMBALI IKIWEMO YA YESU, UNATAKA KUJUA MAANA YA ZILIZOBAKI NA TATTOO ZA MASTAR WENGINE WENYE TATOO? FUNGUA HAPA SASA

messi-jesus-tat
Kuna baadhi ya watu wanaamini Tattoo ni moja kati ya njia za utunzaji kumbukumbu za matukio muhimu mwilini..na wakati mwingine hata kupamba mwili kwa mchoro  wowote anaovutiwa nao mtu.

unajua chadema wamejipangaje ubunge na udiwani mwaka huu?

CHADEMA-LOGO

AJALI YA KILIMANJARO ILIKUWA HIVI,TAZAMA KATIKA PICHA JINSI WATU WANNE WALIVYOPOTEZA MAISHA

>>Ni ajali ya fuso kuigonga hiace 

>>majeruhi 11 wakimbizwa hospitali mawenzi, 

>>watatu ni mahututi

Gari aina ya Hiace iliyogongwa kwa nyumba na Fuso na kuuwa watu huko Moshi

UNADHANI KUMUITA OBAMA NYANI ATAACHE HIVI HIVI? PIA HUU NI UBAGUZI WA RANGI.

Barack-Obama
Rais Barrack Obama
 

Afungwa miaka 8 kwa kumuoza bintiye

 
Raia mmoja wa Australia ambaye alipanga ndoa ya kiislamu li kumuoza bintiye mdogo mwenye umri wa miaka 12 amehukumiwa miaka minane jela.
 
Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 63 alipatikana na mwanamume raia wa Lebanon mwenye umri wa miaka 26 akimuoza bintiye kwake, huku akisema kuwa hakutaka kumuona bintiye akitenda dhambi kwa kufanya ngono nje ya ndoa.
 
Alipatikana na hatia mwezi Aprili kwa kumnadi mtoto kuhusika katika vitendo vya ngono kinyume na sheria.

 
Mapema mwaka huu mume huyo alihukumiwa kifungo cha miaka saba na nusu kwa kumnyanyasa kijinsia mtoto huyo.

 
Msichana huyo mdogo analindwa na serikali.

Thursday, July 16

MTANZANIA WA KWANZA KUPANDA MLIMA EVEREST


MTANZANIA KWENYE KILELE CHA EVEREST
Ni Wilfred Moshi. 
Amekuwa Mtanzania wa kwanza kufika kilele cha mlima mrefu kuliko yote duniani.

Steinmeier ziarani Cuba

Waziri wa Mambo ya Nje ya Ujerumani Frank-Walter Steinmeier leo hii anatarajiwa kuanza ziara yake ya siku mbili nchini Cuba.

Steinmeier außenminister wien  
  Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier


Steinmeir atakuwa waziri wa kwanza wa mambo ya nje wa Ujerumani kufanya ziara nchini humo tangu kuungana tena kwa Ujerumani miaka 25 iliyopita Sudi Mnette anaarifu zaidi.

Monday, July 13

TAARIFA ZA KUSIKITISHA KITUO CHA POLISI STAKISHARI KIMEVAMIWA NA MAJAMBAZI NA KUUA POLISI NAKUPORA BUNDUKI AINA YA SMS USIKU WA KUAMKIA LEO.

WATU KADHAA WAUWAWA, SILAHA ZAPORWA BAADA YA MAJAMBAZI KUVAMIA KITUO KIDOGO CHA POLISI CHA SITAKISHARI, JIJINI DAR ES SALAAM

 
 

ROONEY, BALE?,ANGALIA ORODHA YA WACHEZAJI WA KIINGEREZA WALIOWAHI KUSAJILIWA KWA GHARAMA KUBWA ZAIDI

Ofa iliyokubaliwa ya Manchester City kumsajili kiungo Raheem Sterling kutoka klabu ya Liverpool imeweka rekodi mpya katika orodha ya wachezaji ghali zaidi wenye asili ya taifa la Uingereza.

AUSILIO AKANUSHA TAARIFA ZA INTER KUMWANIA IBRAHIMOVIC

Mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan Piero Ausilio, amethibitisha klabu yake kuwa na mpngo wa kuwasajili Mohamed Salah, Stevan Jovetic na Ivan Perisic - huku akikanusha taarifa zinazowahusisha kumuwania mchezaji wao zamani Zlatan Ibrahimovic na kusema kuwa kwa sasa mchezaji huyo haendani na mipango ya klabu yao.

MAMA WA CASILLAS AAMUA YAISHE NA PORTO

Mama wa Iker Casillas ameamua kuomba radhi kwa kauli yake ya kwamba mwanaye anapaswa kuchezea timu bora zaidi ya Porto.

Afisa usafirishaji ajitosa kuwani Udiwani kata ya Luhota jimbo la Kalenga

KATIBU wa uchumi na fedha wa chama cha usafirishaji Mkoani Iringa, Obedi Luhwago ameamua kujitisa kuwania udiwani katika kata ya Luhota, jimbo la Kalenga wilayani Iringa kwa tiketi ya Chama Cha Mapnduzi (CCM).

PITIA HAPA KURASA ZA MBELE NA NYUMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU, JULAI 13,2015

.

KENYA ,SOMALIA KWAFUKUTA UPYA,KESI YA MIPAKA KUFUNGULIWA NA SOMALIA

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamoud
Serikali ya Somalia leo hii itafungua rasmi kesi dhidi ya kenya katika Mahakama ya kimataifa (ICJ) kufuatia mgogoro wa mpaka baina ya nchi hizo mbili.

I.R.P MZEE OJWANG

Muigizaji maarufu wa kipindi cha runinga cha "Vitimbi"
Benson Wanjau aka "Mzee Ojwang"
ameaga dunia.

Mzee Ojwang ameaga dunia muda mchache uliopita katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta mjini Nairobi Kenya.

RAHEEM STERLING SASA ASHIKA NAMBA TATU KWA WACHEZAJI WENYE THAMANI ZAIDI EPL


STERLING RASMI NI MANCHESTER CITY



Hatimaye klabu za Liverpool na Manchester City zimefikia makubaliano katika sakata la usajili wa kiungo mshambuliaji wa Liverpool, Raheem Sterling na kutua City kwa ada ya uhamisho wa pauni 49m.

TP MAZEMBE YALAZIMISHWA SARE TENA


TP Mazembe imecheza mechi ya pili mfululizo bila ya ushindi, baada ya usiku wa jana kulazimishwa sare ya bila kufungana na wenyeji Moghreb mjini Tetouan, Morocco katika mchezo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Afrika.

Sunday, July 12

SOMA HII ITAKUSAIDIA KUEPUKANA NA UPOTOSHWAJI WA WANASIASA UCHWARA

MUHTASARI WA TAARIFA YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUHUSU UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA MWAKA 2010 HADI  2015  KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO (OKTOBA 2010 HADI JULAI 2015)



-----------------------------------



DKT. JOHN POMBE MAGUFULI

1
Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Dkt. John Pombe Magufuli, mara baada ya kutangazwa kuwa ndiye Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Dodoma Convition Centre, Mjini Dodoma. Dkt. Magufuli ameibuka kidedea kwa jumla ya kura 2104, wakati wapinzani wake Amina Salum Ally, akiibuka na kura 253 na Dkt. Asha-Rose Migiro, akipata kura 59.

MATUKIO MBALI MBALI KWENYE MKUTANO MKUU KATIKA PICHA